ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 15, 2018

PALE WANANCHI WANAPOJITUTUMUA SERIKALI INAWAPIGA TAFU.


 GSENGOtV

Shule ya Msingi Sumbuka ni kati ya shule 139 za msingi zilizojengwa kwa nguvu za wananchi (mafundi, wasombaji maji na nguvu ya mkono kwa mkono)

Shule hii ni moja kati ya shule zilizo na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu, ambapo mahitaji ya vyumba 08 vya madarasa na nyumba za walimu 08.

Mradi wa wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na ofisi moja ya walimu ulianza kutekelezwa mwezi Octoba 2018 na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 3 tangu tarehe ya kuanza. 

Mradi huo utakapokamilika unatarajiwa kupunguza tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa ambao umekuwa hauendani na kasi ya uandikishwaji wanafunzi wapya vilevile utakuwa umeondoa adha kwa wanafunzi waliyokuwa wakiipata kila siku kutembea umbali mrefu kwenda kwenye kata nyingine kupata nafasi jambo ambalo limekuwa chanzo kwa baadhi ya wanafunzi kukatisha masomo.

Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imetoa ufadhili wa Tshs 60,000,000/= kugharamikia ujenzi huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.