ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 9, 2018

*DC MURO AUFYEKELEA MBALI MGOGORO WA ARDHI WA MASHAMBA YA MALULA ARUMERU*

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru *Mhe Jerry Muro* ametatua Mgogoro uliodumu kwa zaidi ya *Miaka Saba*  kati ya wakulima na wafugaji wa kata ya *Malula wilayani Arumeru* na  kuwataka wakulima waendelee kulima katika mashamba ya Malula ambayo ni ardhi ya serikali iliotengwa kwaajili ya uwekezaji wa *viwanda na bandari kavu*

Aidha *Dc Murro* amewataka wanasheria wanaowapotosha wakulima na *wafugaji wa vijiji vya kata ya Malula* kwa kutumia uwepo wa migoogoro ya ardhi kwa njia ya kujinufaisha  kuacha mara moja tabia hiyo na kufuta kesi hizo mahakamani kwani ardhi ni ya serikali na mwenye dhamana na ardhi hiyo ni  *Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli*

*Dc Muro* Amezungumza wakati wa ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa kata ya *MALULA*  ambapo mgogoro huo umetokana na wakulima na wafugaji kufanya maeneo ya mashamba hayo kuwa ya kwao na wengine kupeleka mashtaka mahakamani dhidi ya wananchi walioazimwa maeneo hayo na serikali kwaajili ya kilimo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.