ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, November 13, 2018

MBATIA AELEZA ALICHOZUNGUMZA NA RAIS MAGUFULI IKULU LEO


Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia na Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) amesema kuwa Rais Magufulia amewapokea vizuri na amekubali kuzungumza mambo ya msingi kwa Taifa kwa kuwa waliombwa tangu mwaka juzi.

Mbatia ameyasema hayo mara baada ya kutoka kufanya mazungumzo na Rais Magufu ambapo amesema kuwa wamezungumza masuala ya elimu,afya na Tanzania iwe ya nchi gani.

"Tumezungumza na Mh. mambo ya msingi kwa Taifa letu tulikuwa tumeombwa tangu mwaka jana mwaka juzi sisi ndani ya TCD mimi ni mwenyekiti wao vile vyama vilivyo na uwakilishi Bungeni na vile vyama vile wanaalikwa washirika na kwa kuwa Tanzania ni yetu sote, Tanzania tunashirikiana soteTanzania iliyo njema," amesema Mbatia.

Aidha Mbatia ameongeza kuwa "Rais ametupokea vizuri na kutuhakikishia kwamba yeye yuko tayari tuzungumze vyama vya siasa na Watanzania kwa ujumla, pamoja na viongozi wa dini  ni taasisi ambazo ni sehemu ya Tanzania kwahiyo tukiwa na meza ya mazungumzo na maridhiano ya Kitaifa Tanzania yetu itasonga mbele zaidi na itapata baraka zaidi."

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.