ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 6, 2018

MBUNGE COSATO CHUMI ABANWA NA WANANCHI TATIZO LA UMEME KATIKA KIJIJI CHA RUNGEMBA

Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi akitolea ufafanuzi juu ya swala la tatizo la umeme mara baada ya kupigia simu meneja wa tanesco wilaya ya Mufindi mkoani Iringa

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Wananchi wa kata ya Rungemba mkoani Iringa wamemuweka kikaangoni mbunge wa jimbo la Mafinga mjini Cosato Chumi juu ya kukosekana kwa umeme katika baadhi ya vitongiji ya kata hiyo.

Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara wananchio hao wamesema kuwa wamekuwa walinzi wa umeme ambao umepita katika kijiji cha Rungemba.

“Sisi watu wa Makwawa na Njia Panda tumekuwa walinzi wa huu umeme ambao umepita kwenye hiki kijiji cha Rungemba na kata kwa ujumla maana hakuna hata laini ndogo ambayo inasemekana imepita lakini tumekuwa tunashangaa maana hakuna hata hiyo laini” walisema wananchi hao

Wananchi hao wameendelea kwa kusema kuwa umeme huo toka umefika hauna faida kwa wananchi wa kijiji hicho kwa kuwa wamepelekewa transifoma yenye nguvu ndogo kulingana na mahitaji ya wananchi.

“Tumewekewa transifoma haina uwezo kwa kuwa inashindwa hata kusukuma mashine za kusagia mahindi hivyo inatulazimu kusafiri zaidi ya kilometa saba kwa bodaboda kupata huduma ya kusaga mahindi” alisema wananchi

Aidha wananchi hao wamesema kuwa wapo tayari kulipia nguzo za umeme ili waweze kupata nishati hiyo kwa maendeleo ya wananchi na kijiji hicho.

Naye mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi akaamua kumpigia simu meneja wa tanesco wilaya ya Mufindi Omary Ally kupata ufumbuzi wa tatizo hilo mbele ya wananchi.
“Meneja nimebanwa hapa kwenye mkutano wa hadhara na wananchi juu ya tatizo la umeme hapa Rungemba hali ipoje” aliuliza swali kwa meneja?

Akijibu hoja hizo meneja wa Tanesco wilaya ya Mufindi Omary Ally kuwa kulikuwa kunatatizo la transifoma hiyo baada ya wiki moja watafunga na wananchi watapata nishati ya umeme ya uhakika kabisa

Hata hivyo Ally akawatoa hofu wananchi kwa kuwaahidi kuletea transiafoma ambayo itakidhi mahitaji ya wananchi wa kijiji hicho na kuondokana na kero hiyo ambayo inarudisha nyuma maendeleo.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya wananchi kata ya Rungemba kukaa kwa kipindi cha muda mrefu bila kuwa na huduma hiyo ya umeme.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.