ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 6, 2018

"SIJAWAHI KUNUNUA WALA KUUZA GARI LOLOTE LA KANISA" ASKOFU MKUU WA KANISA LA EAGT

Askofu mkuu wa kanisa la Evangelistic assemblies of God Tanzania (EAGT) Dk.Brown Abell Mwakipesile.
 AMIRI KILAGALILA/GSENGOtV
NJOMBE

Askofu mkuu wa kanisa la Evangelistic assemblies of God Tanzania (EAGT) Dk.Brown Abell Mwakipesile ameendelea kuwa na msimamo wake wa kuto kuhusika hata kidogo na tuhuma za matumizi mabaya ya uongozi zilizokuwa zikielekezwa dhidi yake na baadhi ya viongozi wa kanisa hilo kwa kuuza majengo ya kanisa na kununua magari huku akiwataka waumini wa kanisa hilo kuelewa ukweli wa mambo hayo na kwamba kwa sasa kanisa hilo liko salama na limekwisha kwa kuwa yeye na viongozi wake hawakuhusika kwa lolote.

Askofu mwakipesile aliyazungumza hayo wakati alipokuwa akifundisha wachungaji zaidi ya mia mbili 200 katika semina ya  siku mbili  ya uamsho kwa kanisa iliyowakutanisha wachungaji na maaskofu wa majimbo sita ya Kanda ya Nyanda za juu Kusini Mashariki yaani Jimbo la Iringa, jimbo la Mufindi, Jimbo la Njombe, jimbo la Ludewa, jimbo la Songea pamoja na jimbo Mbinga na kufanyika katika kanisa la EAGT lililopo katika mtaa wa sido jimbo la Njombe mkoani Njombe.

Askofu Mwakipesile amesema yeye binafsi hakuwahi kuhusika na uuzaji wa jengo hata moja na kuwataka wachungaji kufika katika majengo yao yaliyopo mkoani Dar es salaam na kujionea majengo yao kwa kuwa yapo salama.

‘Kwa hiyo mimi nizungumze hapa kwenu nizungumze na ukweli wangu sijawahi kununua gari hata moja ya kanisa nawaambia tena sijawahi kununua gari hata moja la kanisa pamoja na kwamba nilikuwa katibu mkuu, wala Moses kulola marehemu hakuwahi kuniagiza kununua gari la kanisa hata siku moja, sijawahi kumsainia document yeyote msharika au mchungaji ya kununua gari akiwepo aseme’alisema askofu.

Aidha askofu huyo amesema hajawahi kuuza jengo hata moja na kuwatangazia wa chungaji kuanzia leo kutafuta majengo ya Eagt yalipo ili kujionea usalama wa mali zao.

Mnamo Desember 18 mwaka 2017 bodi ya wadhamini ya kanisa la Evangelistic Assembles of God Tanzania EAGT ilitangaza kumsimamisha kazi askofu mkuu wa kanisa hilo Dk.Brown mwakipesile na wenzake akiwemo katibu mkuu mchungaji Leonard mwizarubi na mhasibu mkuu mchungaji Praygod mgonja ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zilizokuwa zikiwakabili.

Aidha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Desemba 21 ilifuta  amri ya kumzuia kwa muda Askofu Mkuu wa Kanisa hilo na wenzake, kujishughulisha na mambo ya kanisa hilo kwa nafasi zao, ikiwemo kufanya miamala kwenye akaunti  ya kanisa.

 Pamoja na kufuta amri hiyo, pia mahakama iliwataka wachungaji waliochaguliwa kuwa viongozi mbadala wa kanisa hilo katika uchaguzi uliofanyika katika mkutano ulioitishwa na mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa kanisa hilo Mchungaji John Mfuko na kufanyika Msimbazi Centre jijini Dar es Salaam, kuacha mara moja kufanya shughuli za uongozi wa EAGT na wakikaidi wakamatwe mara moja.

Katika hatua nyingine kwa kuwa hali ya kanisa hilo imekwisha tengamaa askofu Mwakipesile aliwaeleza wachungaji kuwa walikwishaunda bodi inayoundwa na maaskofu wa kanda tisa kuchunguza mikataba na mapato na kuludisha majibu katika taarifa za wachungaji.

‘Kwa hiyo tulishaunda bodi baada ya kuona wale wenzetu hawaeleiki waende pale wachunguze kilichopo,wachunguze kila kitu waone mikataba halafu baada ya hapo watuletee majibu kwa hiyo tumewaachia maaskofu wa kanda mimi simo na mimi ninangoja taarifa kama ninyi’ alisema.

Aidha pamoja na kukamilika kwa mgogoro huo ndani ya kanisa hilo baadhi ya maaskofu wa majimbo ya kanda ya nyanda za juu kusini mashariki katika taarifa zao kwa askofu mkuu wa kanda wamesema kuwa mgogoro huo ulisababisha sintofahamu kwa waumini na wachungaji huku baadhi yao wakiamua kuhama dhehebu.

Miongoni mwa majimbo yalioathirika kwa kiasi kikubwa ni pamoja na jimbo la Mufindi ambapo katika taarifa ya jimbo hilo iliyosomwa na katibu wa jimbo mchungaji Julius Donald kikoti  kwa askofu wa kanda inaeleza kuwa .

Jimbo la Mufindi liliingia kwenye shida tangia aliyekuwa askofu Flangson ndimbwa kuto kuwa na unyenyekevu na nidhamu kwa uongozi wa kanda, kwani mwezi April mwaka 2017 uongozi wa kanisa uliagiza kufungua kazi ya mungu eneo la MITI A  na baadaye alianza kupiga chenga kufanya kazi hiyo na kupelekea kusimamishwa nafasi hiyo.

Aidha taarifa imeendelea kuonyesha kuwa may 2017 baada ya kusimamishwa nafasi hiyo ndipo migogoro ilipoanza kuathiri jimbo zima kwa maana wachungaji kugawanyika kimitizamo.

Katibu aliendelea kueleza kuwa ilipofika tarehe 8,October 2017 baada ya vikao kufanyika ilipelekea uongozi wa kanda kumrudisha katika nafasi hiyo ambayo aliitumikia kwa mda wa miezi mine tu kwa kuwa mnamo tarehe 23/2/2018 wakiwa katika kikao cha kawaida cha jimbo Askofu Flagnson ndimbwa pamoja na aliyekuwa makamu wake mch.Essau Ngeyekwa waliaga rasmi mbele ya kikao au mkutano wa jimbo kwa madai wao ni wanachama wa upande wa pili wa mdhamini ili kupigania haki za EAGT.

Hata hivyo katibu huyo amesema kuwa licha ya mgogoro mkubwa uliojitokeza katika kanisa hilo kitaifa na sasa umekwisha basi yeye na viongozi wengine wamepata nguvu na na kuanza upya kwa sasa kufanya kazi.

Kwa upande wake Askofu Joseph mbwilo wa jimbo la Njombe ambaye ndie mwenyeji wa mkutano wa semina hiyo ya wachungaji anasema kuwa kilichobaki ni kuyafanyia kazi na kuyasimamia mafundisho yaliyo tolewa na Askofu mkuu ili kuwafnya washirika wadumu katika wokovu na kuwataka washirika kumtegemea mungu kwa kila jambo alilo fanya.

‘Mimi nadhani washirika sasa washirika wendelee kumtumikia bwana na mungu wetu ameshafanya kanisa letu lina amani wasijasahau waendelea kuliombea kanisa letu liwe salama zaidi’alisema.

Naye Askofu wa kanda ya nyanda za juu kusini mashariki Askofu Kayombo anasema kuwa lengo la semina hiyo kwa wachungaji ilikuwa ni matengenezo na marejesho kwa kanisa na hivyo tegemeo kubwa ni kuifanya injili ihubiliwe watu waokolewe  na watu wawe viumbe wapya wasiwe kama zamani na hilo litawezekana kwa umoja wao.

Kuhusu changamoto zilizojitokeza kwa wingi siku za nyuma katika jimbo la Mufindi kama taarifa ilivyoeleza Askofu huyo wa kanda amesema kwa sasa jimbo hilo limepata viongozi wapya na makini na hawategemei vurugu zozote katika jimbo hilo.

‘Kwa sasa hivi kwanza tumechagua uongozi mpya na uongozi makini na tumewapa maelekezo ya kutosha kabisa hatutegemi kama kuta kuwa na vurugu tena pale mufindi nategemea yaani muelekeo mpya na maendeleo mapya ya kanisa pale mufindi hizi vurugu vurugu pale hutaziona tena hilo nakuhakikishia’alisema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.