ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 11, 2018

MBARONI KWA KUMBAKA NA KUMNYONGA MTOTO WA MIAKA NANE





Jeshi la polisi mkoani Mbeya linamshikilia mkazi wa kata ya Upendo wilayani Chunya Masanja Willy (25) kwa tuhuma za kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka minane, Kwangu Bundala ambaye alikuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Upendo kisha kumnyonga na kumuua.

Afisa Mtendaji wa kata ya Upendo, Lucas Alan Mwangala ambaye ndiye aliyetoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo la ubakaji amesema wananchi baada ya kupata taarifa za kubakwa kwa mtoto huyo walishirikiana na polisi kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha kituo cha polisi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.