ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 12, 2018

MANSOOR AFUNGUA BARABARA KWA MSHAHARA WAKE - ZAIDI KM 80



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

Wananchi wa jimbo la kwimba mkoani Mwanza, wamempongeza mhe.Shanif Mansoor, mbunge wa jimbo la kwimba, kwa juhudi zake za kuwaletea maendeleo wakazi wa kata ya shilembo kwa kuwafungulia barabara zaidi ya km.30 kwa kutumia posho ya mshahara wake.

Diwani wa kata ya shilembo mhe.Elias Garula, amesema zaidi ya miaka 5o tangu vijiji hivi viazishwe hawakuwahi kuona barabara wala gari katika maeneo hayo, wananchi wamesema kutokana na changamoto ya barabara, wanawake wengi wamepoteza maisha na watoto hasa wakati wakujifungua, kutokana na ukosefu wa miundombunu ya barabara ambapo magari yalishindwa kufika katika vijiji vya shilembo.

Wananchi wamempongeza MANSOOR, kwa jitihadazake binafsi za kuwafunguliya barabara hiyo,ambazo kwao ilikuwa ni ndoto kwani maendeleo yamechelewa kufika maeneo hayo kutokana na changamoto ya kukosekana kwa  barabara.

Ndalawa Magashi, ni mtendaji wa kata ya shilembo tarafa ya mwamashimba wilayani kwimba mkoani Mwanza, amema,shukuru kubwa kwa mhe.MASOOR,kwa kazi nzuri anayo ifanya kwa wananchi wa jimbo la kwimba, nakusema wabunge wengi wamepita kwenye jimbo la kwimba lakini MANSOOR,ni mbunge wa pekee, maarufu mbunge wa vitendo.

Aidha wanancha wa kata ya shilembo baada ya kuona Greda limefika katika kata hiyo,walionyesha furaha yao huku wakipiga kelele za vifijo na nderemo kwakuona greda limeanza kuchimba barabara hiyo, kwani wanafunzi pia kipindi cha masika wanapatashida kuvuka maeneo korofi na wengine kushindwa kuhudhuriya masomo.

Pia wananchi wa kata shilembo, wameomba serekali kuangalia barabara hiyo kwa jicho la tatu kuiwekea moramu na kalavati ili barabara hiyo iwe ya kudumu na endelevu, kwani itafungua maendeleo katika maeneo hayo vijiji vya shilembo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.