ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, July 12, 2018

NSSF NA MWANZA HUDUMA WAZIKUBALI JUHUDI ZA MBUNGE WA ILEMELA - WAKABIDHI MIFUKO 580 YA SARUJI



ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV
Katika kuimarisha miundombinu ya Elimu, Afya, mazingira na Michezo, Leo Mfuko wa Pesheni kwa Mashirika ya Umma NSSF umekabidhi mifuko 580 ya sariji kwa kituo cha Angelina Foundation ili kuwa sehemu ya usukumaji wa harakati za uboreshaji miundombinu Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza.

Akikabidhi mifuko hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF,  Matson Mwakila ambaye ni Kaimu Meneja Kiongozi wa NSSF Mwanza amesema kuwa sera ya kurudisha fadhila kwa jamii kwa kusaidia miradi ya maendeleo imewasukuma kutimiza hilo sanjari na kuziona juhudi za wazi za Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula, ambaye amekuwa akihangaika usiku na mchana kubuni njia na miradi mbalimbali ili kuwanusuru watu wa Jimbo lake na changamoto walizonazo.
Mfuko wa hifadhi ya Jamii wa NSSF pamoja na Kampuni ya Mwanza Huduma wameamua kumuunga mkono Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula kwa kumkabidhi mifuko mia nane na themanini ya Saruji yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni kumi na tano kwaajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mwakilishi wa mkurugenzi mkuu wa mfuko wa hifadhi ya jamii NSSF ndugu Matson Mwakila amesema kuwa NSSF ni mfuko wa jamii wenye sera ya kurudisha fadhila kwa jamii inayowazunguka kwa kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa jamii ikiwemo miradi ya afya, elimu, michezo na mengineyo yenye umuhimu mkubwa kwa jamii,  Kupitia ombi lililowasilishwa na taasisi yake ya mbunge wa jimbo la Ilemela ya The Angeline Foundation kuamua kusaidia jamii hiyo

‘…  Sisi NSSF tutaendelea kuunga mkono serikali na viongozi wake katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ili kumaliza kero na changamoto zinazoikabili jamii, Pia niwaombe watu wengine kutushirikisha wakati wowote watakapohitaji msaada wetu na mara zote tutaendelea kufanya hivyo …’ Alisema

Kwa upande wake mkurugenzi wa kampuni ya Mwanza Huduma ndugu Zully Nanji mbali na kumhakikishia ushirikiano  mbunge huyo  amesema kuwa kitendo cha kumuunga mkono mbunge huyo si mara ya kwanza na ataendelea kufanya hivyo ili kumaliza kero na changamoto zinazoikabili jamii 

Akihitimisha makabidhiano hayo mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula amewashukuru wadau hao kwa kumuunga mkono huku akiahidi kuitumia saruji hiyo kwa kufyatulia tofali zitakazotumika kukamilisha maboma ya majengo ya madarasa, zahanati au ofisi za taasisi za umma kulingana na mahitaji huku akiwaomba wananchi na viongozi kuendelea kushirikiana.

Makabidhiano hayo yalishuhudiwa na mstahiki meya wa manispaa ya Ilemela Mhe Renatus Mulunga, Kaimu mkurugenzi Daniel Batare na viongozi wengine mbalimbali.


‘ Ilemela ni yetu, tushirikiane kuijenga’

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.