Mvua kubwa imenyesha leo jijini Mwanza, ingawa ilianza majira ya giza totoro saa nane za usiku, ikipiga mdogo mdogo ilikolea zaidi majira ya saa 12 asubuhi nayo ikadumu ikiachia na kurudi hadi saa saba mchana.
Imezua taharuki kwa wakazi wa jiji hili biashara zikisimama, baadhi ya huduma zikishindwa kufanyika kwa utaratibu wake, usafiri ukiwa mgumu na msongamano mkubwa wa vyombo vya usafiri kwenye barabara zetu finyu.
Kamera yetu kwa kiasi chake imejitahidi kuzuru baadhi ya sehemu.....na hizi ndizo taswira.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.