ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 21, 2018

VIDEO;- CHELSEA 1-1 BARCELONA

Barca vs chelsea / 1-1/highlights/ 21 FEB 2018 / Champaions league


NYOTA wa Klabu ya Barcelona na Timu ya Taifa ya Argentina, Lionel Messi, amevunja rekodi ya kutofunga goli lolote dhidi ya Chelsea ya Uingereza pindi timu hizo zinapokutana.

Imemchukua mchezaji kutumia dakika 730 na mechi 9 kufunga bao lake la kwanza katika michuano ya Klabu Bingwa Barani Ulaya (UEFA), ikiwa ni dakika ya 75 ya mchezo usiku wa kuamkia leo.

Messi ambaye amekuwa yuko katika kikosi kimoja na Andres Iniesta tangu aanze kuichezea Barcelona, alikuwa hajawahi kuzitikisa nyavu za Chelsea hata mara moja.

Iniesta ndiye alimsaidia Messi kufunga bao hilo kwa pasi safi ikitokea upande wa kushoto mwa uwanja wa Stamford Bridge na kuizamisha nyavuni fasta.

Bao lake la kusawazisha limekuwa muhimu kwa Barcelona ambayo imekuwa na faida ya goli moja la ugenini, kabla timu hizo hazijakutana tena katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Camp Nou, Jumatano ya Machi 14, 2018.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.