ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 30, 2017

HABARI YA MAWAZIRI WANNE WA UGANDA KUFIKA GEITA KUJIFUNZA UCHIMBAJI MDOGO WA MADINI

Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita aliyevaa miwani na Koti la kijivu akimpokea Waziri wa Madini wa Uganda Mheshimiwa  Lokeris Peter  baada Mkoani Geita na ujembe wa Mawaziri wanne na wanasheria kwa ajili ya kujifunza namna Serikali ya Tanzania inavyowawezesha wachimbaji wadogo, Kati na Wakubwa katika Shughuli zao.
Naibu Waziri wa Madini Mheshimiwa Stanslaus Nyongo Mwenye kizibao cha rangi nyukundu akiwa na viongozi wa Mkoa wa Geita pamoja na Mawaziri wanne wa Serikali ya Uganda baada ya Kuwasili Mkoani Geita kujifunza uchimbaji mdogo, Kati na Mkubwa wa Madini.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel wa kwanza kulia akiwaongoza Mawaziri kutoka Uganda kwenda kukagua shughuli za uchimbaji mdogo Lwamgasa Wilayani Geita.

Mawaziri wanne kutoka kutoka Uganda pamoja na viongozi wengine wa Wizara ya Madini na Mkoa wa Geita wakujionea shughuli za ujenzi wa Kituo cha mfano cha Serikali zinavyoendelea katika eneo la Lwangasa Wilayani Geita. Kituo hiki kinajengwa kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa madini ya Dhahabu.
Naibu Waziri wa Madini Mheshimiwa Stanslaus Nyongo akiongozana na Mawaziri kutoka Uganda pamoja na wataalamu wa Madini kukagua shughuli za uchimbaji mdogo wa madini katika mgodi wa Kadeo Lwamgasa Geita.

Mmiliki wa Mgodi wa KADEO Mine Limited ndugu Kadeo akitoa maelezo kwa Mawaziri na wataalmu wa madini walipotembelea Mgodi wa KADEO Mine kujifunza shughuli za uchimbaji mdogo wa Dhahabu Kata ya Lwamgasa Geita.

Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa Geita mwenye koti la kijivu na miwani akiwaongoza Mawaziri  kutoka Uganda kukagua shughuli za uchimbaji wa madini katika mgodi wa KADEO.

Naibu Waziri wa Madini Mheshimiwa Stanslaus Nyongo akizungumza na wadau wa madini na wanachama wa chama cha wachimbaji wadogo wa madini katika Mgodi wa Busolwa Mine wakati wa zaiara ya mwaziri waane kutoka Uganda ya kujifinza uchimbaji mdogo wa Madini.

Mwaziri kutoka nchini Uganga pamoja na wataalamu wa madini wakifuatilia kwa karibu shughuli za uchimbaji mdogo zinavyofanyika katika Mgodi wa KADEO Limited uliopo kata ya Lwamgasa walipokwenda kujifunza uchimbaji Mdogo.

PICHA ZOTE NA Magesa Jumapili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.