ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 14, 2017

RAIS KENYATTA:- NILIHISI UCHUNGU SANA KWA HATUA YA MAHAKAMA KUFUTA USHINDI WANGU.

Aidha Rais Kenyatta amesema kuwa, hana chuki na jamii ya Wakisii ambayo anatokea Jaji Mkuu David Maraga aliyefuta ushindi wake, ingawa amesisitiza kwamba, anapinga uamuzi wa jaji huyo. "Hebu chukulia kama umenunua ng'ombe kisha akaibwa, hatimaye polisi wakampata na walipompeleka mahakamani jaji akasema kwa sababu fomu ya 'P3' haikujazwa hivyo ng'ombe huyo anatakiwa arejeshwe kwa mwizi."
Jaji Mkuu David Maraga aliyefuta ushindi wa Rais Kenyatta
Akisisitiza kuwa hana chuki na jamii ya Kisii Rais Uhuru Kenyatta amesema: "Sina shida kamwe na jamii ya Kisii lakini nina shida na mahakama na huyo mzee kwa uamuzi wake. Nikikosa kujitetea watu watadhani ni kweli niliiba. Lazima nijitetee, hata wewe ukifanyiwa dhambi sharti ujitetee. Lakini pia hatutaki siasa za ukabila. Hatutaki kurudi huko tena, tulipoteza uhai wa Wakenya na mali zetu. Tukashifu siasa zinazoendeshwa kwa msingi wa ukabila," Alisema Rais Kenyatta

Wakenya wakipiga kura katika uchaguzi wa Agosti nane mwaka huu.
Awali Muungano wa National Super Alliance (NASA) ulipinga ushindi wa Rais Kenyatta aliyepeperusha bendera ya chama cha Jubilee katika uchaguzi wa Agosti nane, ambapo hata hivyo Mahakama ya Kilele ya nchi hiyo ilikubali malalamiko ya muungano huo wa upinzani na kufuta ushindi wake. Katika malalamiko yake mahakamani NASA  ilihoji fomu 34A na 34B kwamba zilikuwa na dosari kwa kutotiwa sahihi na mawakala huku zingine zikikosa kujazwa matokeo kando na kutokuwa na alama za usalama.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.