ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 4, 2017

MWENGE WA UHURU WAMULIKA CHANGAMOTO ZA VIFO VYA UZAZI.



Ili kupunguza vifo vinavyosababishwa na akina mama kujifungulia majumbani kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Amour Hemed Hemed amewataka watu wote wenye utamaduni huo kuachana nao ili kunusuru vifo vitokanavyo na uzazi.

Kiongozi huyo ametoa rai huyo Wilayani Ludewa kwa wakazi wa kijiji cha Madope mara baada ya kuzindua jengo la hospitali ya mama na mtoto lililogharimu zaidi ya shilingi Milioni 37 na kuwataka wanawake wa kijiji hicho wenye utamaduni huo kuelimishana juu ya madhara ya kitendo hicho.

Nao Wakazi wa kijiji cha Madope Wilayani Ludewa Mkoani Njombe ambao wamefanikiwa kujenga zahanati kwa ajili ya kurahisisha huduma za afya kwa kina mama na watoto wamesema wamekuwa wakitembea umbali wa zaidi ya kilomita 20 kupata huduma za afya hali ambayo iliwawia vigumu wajawazito.

Mwenge wa Uhuru umemaliza mbio zake Mkoani Njombe na kukabidhiwa Mkoani Ruvuma ambapo ukiwa mkoani Njombe umekagua, umezindua na kutembelea miradi 55 yenye thamani ya zaidi ya shilingi ya BILIONI 8 na milioni 674.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.