ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 4, 2017

FIBA YARUHUSU MABINTI WA KIIRANI KUSHIRIKI KATIKA MASHINDANO YA KIMATAIFA WAKIWA NA VAZI LA HIJABU


Shirikisho la Mpira wa Kikapu Duniani (FIBA) limetangaza kuafiki pendekezo la Iran la kutaka wanawake wa Kiislamu na mabinti wenye Hijabu wa Kiirani kushiriki katika michezo ya kimataifa ya mpira wa kikapu (basketiboli). 
Mahmoud Mashhoon Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran  ametangaza kuwa, hatimaye Shirikisho la Mpira wa Kikapu Duniani (FIBA) limekubaliana na matakwa ya Iran ya wachezaji wake wa kike kushiriki katika mashindano ya kimataifa ya mpira wa kikapu wakiwa wamejistiri kwa vazi tukufu la Hijabu. 
Ameongeza kuwa, uamuzi huo wa FIBA umetangazwa katika kikao cha shirikisho hilo kilichofanyika huko Hong Kong. Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kufuatia uamuzi huo, kuanzia Oktoba mwaka huu mabinti wa Kiirani sasa wataweza kushiriki katika mashindano ya kimataifa ya mchezo huo wakiwa wamejistiri kwa vazi la Hijabu.

Timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Kikapu ya Jamhuri ya kiislamu ya Iran
Ikumbukwe kuwa, Timu ya Taifa ya Wanawake ya Mpira wa Kikapu ya Jamhuri ya kiislamu ya Iran kwa muda sasa haikuwa ikishiriiki katika mashindano ya kimataifa ya mpira wa kikapu kutokana na Shirikisho la Mpira wa Kikapu Duniani (FIBA) kupiga marufuku wanawake wanaovaa Hijabu kushiriki katika mashindano yanayoandaliwa na shirikisho hilo. 
Shirikisho la Mpira wa Kikapu Duniani (FIBA) lililazimika kuanzisha mchakato wa kuangalia uwezekano wa kuruhusiwa vazi la Hijabu baada ya shirikisho hilo kupokea malalamiko kutoka nchi kadhaa kufuatia marufuku yake ya Hijabu katika mashindano ya kimataifa yanayoandaliwa na shirikisho hilo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.