ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 9, 2017

UMOJA WA AZAKI ZA VIJANA WAKUTANA KUJADILI VIPAUMBELE VYAO KATIKA BAJETI YA 2017/2018

  Mbunge wa viti maalum wa Pwani, Hawa Mchafu Chakoma (CCM) akizungumza kwenye kongamano la vijana kuhusu mchakato wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha na Geofrey Adroph
 Mbunge wa Kasulu Vijijini, Vuma Augustine (CCM) akizungumza na vijana kwenye kongamano lililoandaliwa na Asasi ya Dira ya Vijana (TYVA) kwa kushirikiana na asasi za mbalimbali za vijana katika kujadili vipaumbele vya vijana katika bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kuhusu namna ambavyo wabunge wanajaribu kupigania maslahi ya vijana kwenye bajeti. 

Mbunge wa viti maalum wa Katavi, Rhoda Edward Kunchela(CHADEMA) akizungumza na vijana kuhusu mchakato wa bajeti unavyofanyika kutoka ngazi ya chini mpaka ya juu kwenye kongamano la vijana lililofanyika leo kwenye ukumbi wa Wanyama jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Umoja wa AZAKI akizungumza na vijana kuhusu mchakato wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 leo kwenye ukumbi wa Hoteli ya Wanyama jijini Dar es Salaam leo.
 Mratibu wa Mtandao wa Vijana na Bajeti, Saddam Khalfan akizungumzia suala la bajeti ya taifa hasa kwa bajeti ya mwaka 2017/18 kuwa ni sera na sheria mama ya masuala ya mapato na matumizi ya serikali hivyo serikali ni lazima ifahamu umuhimu wa kuzingatia mahitaji ya vijana na ushirikishwaji wao katika mipango ya maendeleo kwenye kongamano lililowakutanisha vijana leo katika ukumbi wa hoteli ya Wanyama jijini Dar.
Majadiliano yakiendelea kuhusu mchakato wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha  2017/2018 hasa kwa bajeti inayowahusu vijana lililoandaliwa na Asasi ya Dira Vijana (TYVA) kwa kushirikiana na asasi mbalimbali za vijana kwenye hotel ya Wanyama leo jijini Dar es Salaam.  
Baadhi ya vijana wakiwa kwenye kongamano lililowakutanisha ili kujadili masuala ya bajeti hasa bajeti ya mwaka 2017/18 inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Stella Vuzo( katikati) akiwa kwenye kongamano la vijana lililofanyika leo kwenye ukumbi wa hotel ya Wanyama jijini Dar es Salaam leo. Wa kwanza kulia ni Victoria Mwanziva ambaye ni mtafiti wa masuala ya Demokrasia na Maendeleo. 
 Mbunge wa Kasulu Vijijini, Vuma Augustine (CCM) akichokoza mjadala wa bajeti kwa vijana
Baadhi ya vijana wakichangia mada juu ya bajeti kwa vijana pamoja na upatikanaji wa ajira
Mshauri wa Demokrasia na utawala bora, Frederick Fussi akitoa mada kwenye mkutano huo
 Baadhi ya vijana wakiwasilisha maoni
Mbunge Viti Maalum CHADEMA, Anatropia Theonest akifunga kongamano la vijana lililokuwa linajadili mchakato wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018.
 Mbunge wa Kasulu Vijijini Vuma Augustine akizungumza na waandishi wa habari na waandishishi wa habari kuhusu ukusanyaji wa maoni kwenye kipindi hiki cha kuelekea kwenye bujeti ya mwaka 2017/2018.
  Mbunge wa viti maalum wa Katavi Rhoda Edward Kunchela(CHADEMA) jinsi alivyoshiri kwenye mchakato wa vijana kutaka kujua ni kwa jinsi gani vijana wanaweza kunufaika na bujeti ya Taifa.
Makamu wa Rais wa DARUSO, Shamira Mshangama akizungumza na waandishi wa habari kuhusu bujeti zinazowekwa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu pamoja changamoto wanazozipata katika upatikanaji wa fedha za mikopo zinazotengwa na serikali katika bajeti yake.

Mkuu wa Idara ya Mafunzo (TYVA), Dianarose Lyimo akizungumza na waandishi wa habari kuhusi taasisi ya Vijana ya TYVA inavyojihusisha na mijadala pamoja na makongamano kwa vijana kutambua umuhimu wa bajeti hasa bajeti ya Vijana.
Picha ya Pamoja 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.