ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 4, 2016

MBUNGE WA KIBAHA MJINI- KOKA AKABIDHI MADAWATI 537 KWA WATENDAJI WA HALMASHAURI

Mbunge wa jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kushota  akimkabidhi madawati mmoja wa watendaji wa halmashauri ya mji kibaha katika halfa ya makabidhiano yaliyofanyika katika shule ya sekondari miembe saba ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais, ambapo ofisi ya mbunge imetoa madawati 537 yenye thamani ya shiingi milioni 60.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Mbunge wa jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kushoto akiwakabidhi watendaji wa halmashauri madawati katika hafla iliyofanyika katika shule ya sekondari miembe saba.

NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

IMEELEZWA tatizo la   kushuka kwa kiwango cha ufaulu katika baadhi ya shule za msingi na sekondari katika halmashauri ya mji wa Kibaha  lilikuwa linasababishwa na wanafunzi wengine  kujisomea wakiwa wamekaa chini ya sakafu sambamba  na kuwepo katika mazingira ya  miundombinu ambayo sio rafiki kwao hivyo kujikuta wanashindwa kutimiza malengo yao.

Hayo yamebainishwa na  wanafunzi wa shule ya sekondari Miembe saba waliohudhuria katika halfa fupi  za ugawaji wa madawati ambayo yametolewa na Ofisi ya  Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka ikiwa ni  utekelezaji wa agizo la Rais Dr. John Magufuli la wanafunzi wote nchini kuhakikisha wanasoma wakiwa wamekaa kwenye madawati.

 Wanafunzi hao akiwemo Ayoub Joseph,Paul Kisige pamoja na Riziki Ismail walisema kwamba kitendo cha baadhi yao kujisomea wakiwa sakafuni kimepelekea kupunguza uwezo wa kifikiri na kujikuta wanafanya vibaya katika masamo yao na kushindwa kufaulu, hivyo wameipongeza serikali  ya Rais Dr John Pombe Magufuli kwa juhudi wanazozifanya za kupambana na adha ya  madawati.

Hapo mwanzoni kwa kweli hali ilikuwa ni ngumu sana kwa sababu wanafunzi wengine walikuwa wansoma wakiwa wanakaa chini ya sakafu na hii kiukweli unamwondolea kabisa uwezo wa kufanya vizuri mwanafunzi, lakini kutokana na agizo hili la Rais tumepata nafuu kubwa na wanafunzi tuna imani tutaweza kufanya vizuri katika masomo yetu, na pia tunampongeza mbunge wetu kwa juhudi zake za kutuletea madawati,”walisema wanafunzi hao.

Pia walisema kwamba pamoja na changamoto ya kuwepo kwa upungufu wa madawati lakini serikali inatakiwa kuhakikisha inatilia mkazo suala linguine la nyumba za walimu pamoja na kuimarisha mambo mengine ya msingi, kama kuongeza madarasa mwengine ili kuweza kuepukana na mlundikano kwa wanafunzi.

 Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka  katika hotuba yake ya kukabidhi madawati hayo amewataka wanafunzi pamoja na walimu kuachana na tabia ya kuhujumu na kuiharibu  miundombinu ya shule na badala yake wahakikishe wanatunza mali zote za serikali kwa lengo la kuweza  kuwasaidia watoto wengine wa vizazi vijavyo waweze kusoma katika mazingira mazuri.

Aidha Koka katika hatua nyingine amebainisha kwamba madawati hayo 537 ambayo ameyatoa katika jimbo lake yataweza kuwa mkombozi mkubwa kutokana na kuweza kuwasaidia wanafunzi zaidi ya 1600 waliokuwa wanakabiliwa na chanagamoto ya kusoma katika mlundikano mkubwa na baadhi yao walikuwa  wanakaa chini ya sakafu.

Naye Afisa elimu wa shule za msingi katika  halmashauri ya mji Kibaha Maajabu Nkanyemka amesema kwamba kwa sasa hawana mapungufu yoyote ya madawati hivyo  hakutakuwa na changamoto ya mwanafunzi wake kujisomea wakiwa wamekaa chini ya sakafu.

MADAWATI hayo 537 ambayo yametolewa na ofisi ya Mbunge wa Kibaha Mji yamegharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 60 yatasambazwa katika kata zote 14 ambapo pia yataweza  kusaidia kwa kiasi kikubwa kuwaondolea adha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ambao walikuwa wanakabiliwa na changamoto hiyo kwa kipindi cha muda mrefu na hatimaye  kuongeza kiwango cha ufaulu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.