ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 6, 2016

MAHAKAMA KUU YATUPILIA MBALI RUFAA ILIYOLETWA NA MWENDESHA MASHTAKA WA SERIKALI (DPP) KESI YA ALIYEKUWA KAMISHNA MKUU WA TRA NA WENZAKE.

 Aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ‘TRA’, Harry Kitilya, Sioi Solomoni na aliyekuwa afisa mwandamizi benki ya Stanibic tawi la Tanzania ambaye pia ni mshindi wa taji la Miss Tanzania 1996, Shose Sinare wamefika Mahakama kuu leo May 06 2016 ili kusikiliza rufaa ya kufutiwa shitaka namba nane la utakatishaji fedha.

Rufani hiyo imesikilizwa leo ambapo mahakama kuu imefuta pingamizi hilo kutokana na kuwa na dosari hivyo shauri linarudi kwenye mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kuendelea pale lilipokuwa limeishia na upande wa Jamhuri wanaweza kuandaa tena rufani na kufungua tena.

Serikali ilikuwa imekata Rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia washitakiwa shitaka  la kutakatisha pesa ambalo liliwafanya wanyimwe dhamana.

Baada ya shitaka hilo kufutwa, watuhumiwa sasa wanaweza kuomba dhamana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.