ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 29, 2016

VIONGOZI WA SIASA,WAFANYABIASHARA WATAKIWA KUWATHAMINI WALEMAVU

 Kaimu katibu  mkuu wa UVCCM taifa Shaka Hamdu shaka akiwa anapokea risala kutoka kwa moja wa mwanafunzi  mlemavu wa viungo.


 kaimu katibu mkuu akiwa anaangalia jinsi mtoto ambaye ni mlemavu  wa akili alivyoandika katika karatasi yake


 mmoja wa mtoto ambaye ni mlemavu wa viungo akiwa anasoma risala fupi mbele ya mgne rasmi


 mkuu wa shule ya msingi  Mreyai  Nuruel Laizer akiwa anampa maelekezo ya ujenzi wa choo cha watoto wenye ulemavu kaimu katibu mkuu wa UVCCM taifa


 kaimu katibu mkuu wa UVCCM  taifa akiwa anakata mti tayari kwa kupanda katika shule ya watoto wenye ulemavu



 kaimu katibu mkuu wa uvccm taifa shaka hamdu  shaka akiwa amembeba mmoja ya mtoto mwenye ulemavu wa akili
 Na Woinde  Shizza, Rombo
Viongozi wa kisiasa, wafanyabiashara, viongozi wa kiserikali na wafanyajazi
wametakiwa kuwajali na kuwathamini sana watoto  wenye ulemavu na wanaoishi
kwenye mazingira magumu kwani wao pia  ni binadamu wanao sitahili kupata
haki na mahitajj muhimu ya kibinadsmu
Hayo yamebainishwa na leo na kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu
Shaka wakati alipotembelea shule ya msingi Mreyai iliyopo wilayani Rombo
mkoani Kilimanjaro yenye jua huduma watoto wenye ulemavu wa viungo na MTI
ndio wa akili.
Alisema kuwa ni muhimu kuwajali sana watoto wenye ulemavu kwani
wakitengenezwa vizuri na kuandaliwa vizuri kwa kupewa elimu  watakuwa
viongozi wazuri wa baadae.
Aidha alivitaka vyama Vya siasa vijielekeze kutatua changamoto na ma tatizo
ya watoto ambao ni Walemavu na sio kuendeleza Kufanya siasa ata sehemu
ambayo aitakiwi siasa.
"napenda kuviambia vyama vingine vya siasa sasa ivi uchaguzi imeisha ni
kipindi cha kufanya kazi na kuachana na siasa sasa ivi ni kipindi cha
kufanya kazi na kutatua ma tatizo ya wananchi " alisema Shaka.
Kwa upande wa Mkuu wa shule ya msingi Mreyai, Nuruel Laizer alisema kuwa
shule hiyo inahudumia wanafunzi wenye Mtindio wa akili na wanafunzi ambao
ni walemavu wa viungo ambapo alisema kuwa shule hiyo inakabiliwa na
changamoto mbalimbali ikiwemo ya ukosefu wa chakula cha wanafunzi, ukosefu
wa vitanda na mgodoro ya kulalia Wanafunzi ambao ni walemavu ,baskeli kwa
ajili ya watoto ambao ni walemavu wa miguu.
Alisema kuwa Wanafunzi hao wanakaa katika ma bweni apo shule ni lakini
wanaupungufu mkubwa wa vitanda na mgodoro  kwani vitanda ambavyo wana vitu
mia wameviazima kutoka kwa watu na mda wowote wenyewe wanaweza kuja
kuchukuwa.
Aliomba serekali pamoja na wadau mbalimbali kujitokeza kuwasaidia kitu icho
ili watoto hao waweze kuishi kwa amani na furaha kama watoto.
"watoto hawa wanawazazi lakini wazazi hao hawana uwezo na ndio maana wa me
wamewaleta Hapa ili wapate elimu hivyo tu naomba sana serekali na wadau
mbalimbali wajitokeze kutusaidia"alisema laizer
Shule hii ya msingi Mreyai imepata msaada wa chakula, maharage, malindi,
sabuni, mafuta, miswaki na kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu
Shaka aliaidi kusaidia shule hii vitanda Nane na mgodoro kwa ajili ya
wanafunzi hawa wenye ulemavu wa viungo pamoja na Mtindio wa ubongo.
kaimu katibu mkuu wa uvccm taifa akiwa anaongea na wanafunzi wa shule ya msingi Mreyai



mkuu wa shule ya msingi Mreyai Nuruel Laizer  wa kwanza kushoto akifuatiwa na mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa kilimanjaro Juma Rahibu Juma akifuatiwa na kaimu  katibu mkuu UVCCM taifa katika makabidhiano ya baadhi  ya msaada ambao ulipelekwa shuleni hapo


 kaimu katibu mkuu akiwa na wanafunzi
 Omary ngwanangwelu akiwa anasalimiana na mmoja wa mtoto ambaye ni mlemavu wa akili

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.