ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 28, 2016

HIVI NDIVYO MWILI WA PAPA WEMBA ULIVYOPOKELEWA DRC.

Maelfu ya watu wamekusanyika leo nje ya uwanja wa ndege wa Kinshasa kuupokea mwili wa mwanamuziki Papa Wemba uliowasili nchini humo kutoka Abidjan
Mwanamuziki huyo ambaye ametajwa kuwa mmoja ya waanzilishi wa muziki wa kizazi kipya cha Soukous anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne baada ya mwili huo kuwekwa katika uwanja wa mpira kwa raia kutoa heshima zao za mwisho.
Mjane wa marehemu, Mama - Marie Lozolo Amazone akisaidiwa na baadhi ya wanafamilia wake pamoja na maafisa kadhaa wa Serikali wakati akiwasili mjini Kinshansa. 
 Maafisa wa serikali na wanadiplomasia watahudhuria ibada ya kumkumbuka mwanamuziki huyo katika uwanja wa ndege kabla ya mwili huo kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Maelfu ya watu wamekongamana nje ya uwanja wa ndege wa Kinshasa kuupokea mwili wa mwanamuziki Papa Wemba uliowasili nchini humo kutoka Abidjan
Hata eneo la daraja kuu mjini humo lilijaa umati mkubwa almuradi tu kutoa heshima zao kwa mwili wa mwanamuziki Papa Wemba uliowasili nchini humo kutoka Abidjan
Mwili wa Marehemu Papa Wemba umepokelewa pia umati mkubwa wa wanamuziki wengine wakiwa sehemu ya kamati ya mazishi ya nyota huyo Nyoka Longo, Malaika Munan, Koffi olomide, Werra son, Tshala Muana, Fally Ipupa na jamaa aliyekuwa swahiba mkubwa wa Papa Wemba mwanamuziki Reddy Amisi.
Kwa mujibu wa mmoja wa wasemaji wa Familia, amesema kuwa Papa Wemba alikuwa nje ya shughuli za muziki wa majukwaa kwa kipindi kirefu akipata matibabu mjini Paris kabla ya afya yake kutengemaa na hatimaye kuhudhuria tamasha kubwa la Burudani huko Abijan. Kifo chake kimeleta mshtuko kwa wengi. 
Mkongwe mkali mwingine aliyefanya kazi kipindi kirefu na Papa Wemba kwa karibu Nyboma Mwandidi katika zama hizi za kuelekea kuusitiri mwili wa rafiki yao ili kumuenzi wamepanga kuvaa kama alivyopenda kuvaa nguli huyo aliye tangulia mbele za haki.  
“We want to celebrate what Papa Wemba was known to promote in terms of attire and music,” he said.
Similar gatherings will be held in London, Brussels and Nairobi led by promoters JC Motindo and Jules Nsana, and Ms Paulin Wanga, a fan.
Tamasha la bure la usiku kucha lilifanyika mjini Abidjan ambapo mwanamuziki huyo alianguka alipokuwa akiimba. Mwanahabari wa BBC Tamasin Ford anasema kuwa mashabiki wengi walivalia nguo nyeusi na kubeba mishumaa ili kutoa heshima kwa nguli huyo wa muziki.

PICHA ZOTE NA http://news.abidjan.net/

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.