ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 19, 2016

HADI SASA WATU 100 WAMENUFAIKA NA AIRTEL MKWANJIKA.

Meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando akikabidhi shilingi 790,000 bw, kwa Elias Makani mshindi wa Airtel Mkwanjika ikiwa ni zawadi yake  aliyojizolea katika boxi la Airtel  Mkwanjika mkoani Dodoma jana, anaeshudia katikati ni Afisa Masoko kanda ya Kati bw, Hendrick Bruno. Promosheni ya Airtel Mkwanjika bado inaendelea ambapo hadi sasa tayari Airtel imeshawanyakua washindi 100 na kuwazawadia pesa taslim kila mmoja.
Meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando akikabidhi shilingi 910,000 kwa Bi  Devota Fongonyo mshindi wa Airtel Mkwanjika ikiwa ni zawadi yake  aliyojizolea katika boxi la Airtel  Mkwanjika mkoani Dodoma jana, anaeshuhudia kulia ni mtangazaji wa kipindi cha mkwanjika Bw Godfrey Rugalabamu (gala B). Promosheni ya Airtel Mkwanjika bado inaendelea ambapo hadi sasa tayari Airtel im
Toka Kulia ni Meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando na mtangazaji wa kipindi cha mkwanjika Bw Godfrey Rugalabamu (gala B) wakwanza kushoto wakisaidiana kuhesabu hela na mshindi wa promosheni ya Airtel Mkwanjika  mkoani Dodoma bw Rioba Matiku ikiwa ni zawadi yake  aliyojizolea katika boxi la Airtel  Mkwanjika mkoani Dodoma jana, Promosheni ya Airtel Mkwanjika bado inaendelea ambapo hadi sasa tayari Airtel imeshawanyakua washindi 100 na kuwazawadia pesa taslim kila mmoja.

AIRTEL MKWANJIKA YAWAZADIA 100 HADI SASA
Airtel Mkwanjika tayari imeshawazawadia jumla ya watanzanzia 100 tangu ilipozinduliwa ambapo jana washindi wengine watatu kati ya saba wa Airtel toka mikoa ya Singida,Dodoma na Tabora, wamevuna fedha katika boxi la promosheni ya 'Airtel Mkwanjika' wakati Boxi la Mkwanjika lilipofika mkoani Dodoma kwa lengo la kuwazawadia washindi wake wa kanda ya Kati.

Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando alisema hayo katika  droo iliyochezeshwa  mjini Dodoma jana kwa wateja  wa kanda  ya kati ambapo wateja wanne wameshindwa kufika licha ya kuambiwa watagharamikiwa kila kitu ikiwemo nauli, chakula na malazi ili waweze kufika kujizolea fedha lakini wamekuwa hawaamini na kuhofia kuwa inawezekana ni matapeli.

"leo wateja wa Singida,Dodoma na Tabora,  ni zamu yenu kujizolea mapesa ya Airtel Mkwanjika, pia natoa wito kwenu wateja wa airtel mnapopigiwa simu za ushindi kwa namba ya Airtel 0683-442244 kutoa ushirikiano kwakuwa droo hiyo haina tozo ya aina yoyote laisema mmbando”.

Mmbando alisema Airtel imetenga kiasi cha sh.milioni 300 kwaajili ya wateja wa Airtel na kila mmoja anaweza kushinda na mteja anachotakiwa kufanya ni kujiunga na kifurushi chochote cha yatosha au kuongeza salio kwa kutumia vocha na kuingizwa moja kwa moja kwenye droo ya siku bila makato yoyote.

Alisema kila siku wateja wanne wa airtel wanavuta mkwanja katika promosheni hiyo na huchezeshwa kila baada ya siku saba za wiki na kutoa washindi 28.

Alibainisha bado zaidi ya wateja 200 kushindaniwa  kwenye bado droo tisa zilizobaki ambazo zitawapa  fursa wateja wanne wa airtel kila siku kushinda kila mmoja hadi sh.milioni moja.

Wakizungumza mara baada ya kujiokotea fedha katika droo hiyo, mshindi wa kwanza mkazi wa Dodoma,James Ryoba matiku, alisema ameweza kujipatia Shilingi laki tisa na elfu kumi ambazo zitamsaidia kuongeza mtaji katika biashara zake za nguo.

Kwa upande wake, Mkazi wa Tabora, Devota Fongonyo, alisema awali alipopigiwa simu ya ushindi hakuamini na kuona kuwa ni matapeli lakini baada ya siku nne alipigiwa tena na akubali kufika Dodoma huku akiwa na hofu.

Alisema katika droo hiyo amejipatia kiasi cha shilingi laki tisa na elfu thelasini ambazo zitamsaidia kulipa ada za watoto wake.

Naye Mkazi wa Kongwa, Elias Makani, alisema amejipatia kiasi cha shilingi laki Saba na elfu tisini ambazo zitamsaidia katika shughuli zake za kilimo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.