ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 13, 2015

WABUNGE MH,MBATIA NA MH,MREMA WAKUTANA KATIKA IBADA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU BABA ASKOFU STEPHANO MOSHI.

Mbunge wa kuteuliwa na rais,Jmaes Mbatia akizungumza jambo na mbunge wa jimbo la Vunjo ,Agustino Mrema mara baada ya kukutana kwa mara ya kwanza jimboni humo katika ibada ya kumbukumbu ya askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini iliyofanyika mwishoni mwa wiki/
Kanisala la KKKT ,Usharika wa Mamba Kotelailokofanyika ibada hiyo
Mbunge Mbatia akiingia kanisani humo.
Ujenzi wa taasisi ya saratani ya Bishop Moshiunaofanyika kando ya Usharika huo.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Bishop Moshi wakiwa katika ibada hiyo.
Viongozi mbalimbali wa dini pia walikuwepo.
Mbunge Mrema akiwa ameketi na mbunge mwenzake Mbatia wakifuatilia ibada hiyo.
Askofu mstaafu Dkt Martin Shao akizungumza wakati wa ibada hiyo.
BabaAskofu Dkt Fredrick Shoo akiongoza ibada hiyo ya kumbukumbu ya miaka 29 ya kifo cha aliyekuwa askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini,Stephano Moshi.
Askofu mstaafu Dkt Erasto Kweka akimzungumzia marehemu Baba Askofu Stephano Moshi jinsi alivyo mfahamu.
Baba Askofu Dkt Shoo akitoa hotuba yake .
Ikafika wakati wa kuchangia ujenzi wa taasisi ya saratani ya Bishop Moshi na aliyealikwamwanzo alikuwa ni Mbunge wa jimbo hilo Dkt  Mrema .
Dkt Mrema akimtizama mkewe Rose Mrema wakati akitoa pesa kwa ajili ya mchango wa harambee ya kuchangia taasisi hiyo ambapo alitoa kiasi cha sh 500,000.
Baadae ikafika zamu ya Mbatia ambaye alipata nafasi ya kuzungumzakido huku akieleza kuwa tayari amekwisha changia kiasi cha Sh Mil 10 kwa ajili ya shule ya sekondari ya Bishop Moshi na pia alitoa kiasi cha sh Mil 2 kwa ajii ya ujenzi wa taasisi hiyo.
Baba Askofu ,Dkt Shoo akimhukuru Mbatia kwa mchango anaoendelea kutoa kwa kanisa.
Baba Askofu Dkt Shoo akizindua rasmi jengo la kuweka kumbukumbu za Askofu wa Kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini Stephano Moshi.
Baba Askofu Dkt Shoo akiingia katika jengo hilo.
Baba Askofu Dkt Shoo akitia saini katika kitabu cha kumbukumbu.
Baba Askofu,Dkt Shoo akiweka shada la maua katika kaburi la askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaskazini na kufanya maombi katika kaburi hilo.
Mbunge wa kuteuliwa na rais,James Mbatia akitia saini katika kitabu cha kumbukumbu ya askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya Kaslazini mStephano Moshi .
Mbunge wa kuteuliwa ,James Mbatia akiweka shada la mauakatika kaburi la Askofu wa kwanza wa KKKT dayosisi ya kasakzini ,hayati Stephano Moshi.
Maaskofu wastaafu ,Dkt Erasto Kweka na Dkt Martini Shao wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa kuteuliwa James Mbatia mara baada ya kumalizika kwa ibada ya kumbu kumbu ya asakofo wa kwanza wa KKKT ,Stephano Moshi.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kasakazini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.