ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 31, 2015

ZAMA HIZI USISHANGAE KULA NYAMA TAMU TBL WANAFANYA YAO.

Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Kilwa Road jijini Dar es Salaam, Lucas Mgaya (wapilikushoto) akimkabidhi kikombe mchoma nyama mkuu wa Bar Chamanzi, Shaban Seif mara baada ya kuibuka mabingwa katika mashindano ya Safari Nyama Choma kitongoji cha Dar One Temeke Dar es Salaam yaliyofanyika katika Uwanja TCC Chang’ombe mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja wa bia ya Safari Lger, Edith Bebwa.

Wachoma Nyama Dar wapewa mafunzo.
Na Mwandishi Wetu.
ZAIDI ya wachoma Nyama na wamilikiwa Bar 143waTemeke, Ilala na Kinondoni jijini Dar es Salaam wamepewa mafunzo ya uchomaji nyama ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mashindano ya Safari Nyama Choma 2015.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti wakati wa mafunzo hayo, Jaji Mkuu wa mashindano hayo , Manase Mwasha alisema lengo la Kampuni ya Bia Nchini (TBL) kwenye mashindano ya Safari Lager Nyama Choma ni kuongeza hamasa kwa watayarishaji na walaji wa nyama choma ili kwa pamoja waweze kufahamu viwango bora vya uchomaji na utayarishaji wa nyama choma.

Alisema Manase, wachoma nyama katika baa za mikoa yote inayoshiriki wanapata elimu na ueledi wa kutosha katika fani hii ili kumpa mlaji ubora anaostahili kila anapokula nyama choma. Tumezingatia maombi ya washiriki mwaka jana hivyo basi mwaka huu semina inayoelekeza namna nzuri ya uchomaji nyama itafanyika kwa bar zote zinazoshiriki na wala sio baa chache zilizochaguliwa kama ilivyokuwa kwa miaka ya nyuma. 

Aliendelea kufafanua  Jaji Mkuu Manase, washiriki watapimwa ujuzi wao katika kutayarisha nyama choma za aina tatu; nyama ya ng’ombe, nyama ya mbuzi na nyama ya kuku.

Manase Mwasha alisema katika mafunzo hayo alisisitiza zaidi vitu muhimu watakavyoangalia katika fainali za kumpata mchoma nyama bora wa mkoa kama usafi, vifaa vya kufanyia kazi, joto maalumu lakuhifadhi nyama na joto maalum la uchomaji nyama. 

Tayari mikoa ya Mbeya, Mwanza, Aresha na Kilimanjaro wameshapewa elimu hii ya Uchomaji Nyama ili kuelekea katika fainali za kumpata bingwa wa kila mkoa katika mikoa shiriki ya mashindano ya Safari Lager Nyama Choma 2015.

Mikoa inayoshiriki fainali za mashindano ya Safari Lager Nyama Choma 2015 ni Mbeya, Mwanza, Arusha, Kilimanjaro na Dar es Salaam.

Bingwa wa mkoa katika kila mkoa atajinyakulia zawadi ya kikombe na pesa taslimu milioni moja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.