SAFARI
LAGER WEZESHWA MSIMU WA IV YATANGAZWA MWISHO WA KUJESHA FOMU.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA
HABARI
Dar es Salaam, Alhamisi
12 Februari, 2015:
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza tarehe
ya mwisho ya kurejesha fomu za programu yake ya Safari Lager Wezeshwa kwa msimu wa nne kwa
wajasiriamali wadogo wadogo na wa
kati Nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja
wa bia ya Safari Lager Bi. Edith Bebwa alisema,
“ Ijumaa tarehe 20 Februari ni siku ya mwisho ya
kurudisha fomu za wanaotaka kujiunga na programu ya Safari Lager Wezeshwa .
Alisema Edith tunawakumbusha wale mliochukua fomu na hamjarudisha basi
mtumie muda huu kuziresha fomu mahala mlipochukulia na kwa wale ambao
hamjachukua bado tuna muda wa takribani siku saba za kuchukua fomu kujaza na kuiresha
ulipochukulia.
Fomu za ushiriki zitapatikana kwenye mabohari
ya TBL, Mawakalai wa kusambaza bia za TBL, kwenye mtandao wa www.wezeshwa.co.tz . Fomu hizo
zichukuliwe, zijazwe na kurejeshwa kwenye vituo vilivyotajwa hapo juu au kwa
njia ya posta kwa sanduku la posta (Safari Lager Wezeshwa msimu wa nne,TBL Dar
es Salaam,P.O Box 9013 DSM), kabla ya tarehe 20 Februari 2015.
Programu hii inafanyika takribani mikoa yote ambapo itawapa fursa
wajasiriamali wa aina zote bila kujali fani,kabila wala jinsia kujaza fomu kwa usahihi na kamilifu kisha
kuzirudisha mahala husika na baadae waliokidhi nafasi zinazohitajika
kuchaguliwa kisha kupewa mafunzo mafupi
pamoja na kukabidhiwa ruzuku zao.
Nae kiongozi wa wataalamu wa ushauri wa biashara kutoka kampuni ya TAPBDS,
Bwana Joseph Migunda alisema kuwa “Zoezi
hili linahusisha wataalamu wenye uwezo na uzoefu mkubwa katika kushauri na
kusaidia ukuzaji wa sekta ya biashara ndogo na kubwa. Hivyo aliomba
wajasiriamali wote kuitumia fursa hii kushiriki kwa kuzingatia vigezo
vilivyoainishwa kwenye fomu ya ushiriki. Wenye nia ya kufika mbali kibiashara
na wenye malengo ya kuisaidia jamii
inayowazunguka wasisite kuchangamkia fursa hii”.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.