ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 3, 2014

MENEJA WA VILLA PARK MWANZA RAMADHAN HUSSEIN ALIPOCHUKUA JIKO LAKE MWISHONI MWA WIKI JIJINI DAR

 Rama na mkewe Husna Mlanzi ambaye ni mtangazaji wa Star Tv.
 Ramadhan Hussein, meneja wa ukumbi maarufu jijini Mwanza, Villa Park jana mchana alifunga pingu za maisha na Husna Salum, ndoa iliyofungwa maeneo ya Ukonga jijini Dar es Salaam.
Ilikuwa ni shughuli iliyofana na kuhudhuriwa na watu wengi, ikiwa ni mwanzo wa kuelekea sherehe kubwa ya harusi yao itakayofanyika baadae huko Mwanza.
Rama amekuwa ni kiungo muhimu wa maonyesho mengi ya muziki, si Mwanza tu bali ni kanda nzima ya ziwa kwa ujumla wake.
GSENGO BLOG inamtakia Rama na mkewe Husna kila la kheri katika maisha yao ya ndoa.


Bi. Harusi Husna Mlanzi ambaye ni mfanyakazi wa Star Tv.
Dua baada ya ndoa kufungwa.
Rama akipongezwa baada ya kufunga ndoa, kushoto kabisa ni Best Man wake Said Mussa.
Picha ya pamoja na bwana harusi.
Marafiki wakubwa wa maharusi waliowakilisha harusini Muhksin Mambo aka Mc Stepper (R) akiwa na mtangazaji wa Star Tv Fatma Shemweta (L).
Rama akifurahia kuwaona marafiki.
Haya sasa kaa mkao wa kula kwani siku ya ijumaa nazungumzia mwishoni mwa wiki hii kutakuwa na Bo-Bo-bonge la party jijini Mwanza la kuwakaribisha maharusi.
Jeh. Unakadi.....!!!?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.