ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 31, 2014

KITUO CHA HABARI CHA UMOJA WA MATAIFA WASHIRIKI ALHAMISI YA BURUDANI NA KIKUNDI CHA MTANDAO WA VIJANA TEMEKE


 Afisa habari wa Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi Stella Vuzo akitoa mada kuu iliyokuwa inahusu malengo ya maendelea ya milenia na kuangalia imefikia wapi kwenye malengo hayo pamoja na kuwaelimisha kuhusu maendeleo endelevu baada ya mwaka 2015(Post 2015 Sustainable Development) iliyotolewa kwa Mtandao wa vijana wa Temeke.

Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa jana iliandaa Alhamisi ya Burudani kwa ajili ya kujifunza kazi mbalimbali za Umoja wa Mataifa. Kwa kila Alhamis ya mwisho wa mwezi Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa huandaa burudani kwa makundi mbalimbali na kujifunza kazi mbalimbali za Umoja wa Mataifa. Alhamisi ya mwezi wa kumi kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa kilitembelea Mtandao wa Vijana wa temeke na kujadili mambo makuu ya malengo ya Milenia pamoja na kuangalia ni jinsi gani vijana wanashiriki katika shughuri za kimaendeleo katika jamii zao
 Mkutubi - Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, Bi Harriet Macha akisisitiza jambo kwenye mada kuu iliyokuwa inahusu malengo ya maendelea ya milenia na kuangalia imefikia wapi kwenye malengo hayo pamoja na kuwaelimisha kuhusu maendeleo endelevubaada ya mwaka 2015(Post 2015 Sustainable Development)
 Mwenyekiti wa Kituo cha Vijana wa Makangalawe, Bwana  Ismael Mnikite akizungumza jambo kuhusu mada husika na kuangalia ni njia  gani zinaweza kuwapelekea vijana kushiriki kwenye shughuli nzima za maendeleo
Mwenyekiti wa Kituo cha Vijana wa Makangalawe, Bwana  Ismael Mnikite akigawa vipeperushi vya Umoja wa mataifa pamoja na fomu kwa vijana hao wa Temeke.
Mada ikiendelea
Katibu wa Mtandao wa Vijana Temeke, Bwana Yusuph Kutengwa akichangia mada
 Omari A. Mketo akichangia
 Ishengoma ambaye ni mlemavu wa macho akieleza faida alizozipata baada ya kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa kutoa mafunzo hayo kwa mtandao wa vijana wa Temeke.

Baadhi ya vijana wa mtandao wa vijana wa Temeke wakisoma kwa umakini malengo ya milenia wakati kituo cha habari cha umoja wa mataifa walipokuwa wanatoa mada kwa vijana hao
Picha ya pamoja

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.