ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 13, 2014

SHINYANGA WALIVYO SAMBAZA UPENDO NA SERENGETI FIESTA

Pichani kati msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka THT,Rachael akiwa na madansa wake wakilishambulia jukwaa kwa namna ya kipekee usiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga.
Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,atambulikae kwa jina la kisanii Ommy Dimpo akiwaimbisha mashabiki huku akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na wakazi wa mji huo usiku katika tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage
Mmoja wa wasanii wa Bongofleva anaefanya vyema katika muziki huo atambulikae kwa jina la Young Killer a.k.a Msodoki akiimba jukwaani kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga

Pichani juu na chini ni umati wa wakazi wa mji wa Shinyanga waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage,usiku wa kuamkia leo.
Wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Ney Wa Mitego (pichani kulia) na Stamina wakilishambulia jukwaa kwa wimbo wao wa Huko Kwenu vipi,huku makele ya shangwe yakiwa yametawala kila kona ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga usiku.
Sehemu ya mashabiki wa Fiesta wakishangilia yaliyokuwa yakijiri kwenye jukwaa la Fiesta 2014 ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga.
Mwanadada Linah akionesha umahiri wake wa kucheza wimbo wake wa Ole Temba juu ya jukwaa la Fiesta 2014 usiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage.
Ukipenda muite Mr Blue,msanii wa muziki wa kizazi kipya juu ya jukwaa la Fiesta 2014 ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage mjini Shinyanga.
Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,atambulikae kwa jina la kisanii Ommy Dimpo akiimba mbele ya mashabiki wimbo wake wa ani kama mama katika tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage
Wanajiita Wakata Mkaa kutoka kundi la Wanaume TMK,Chege na Temba kwa pamoja wakilishambulia jukwa la fiesta mbele ya umati wa watu (hawapo pichani) ndani ya tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja mdodogo wa Kambarage mjini Shinyanga.
Wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Khadija anaetamba na wimbo wake wa maumivu akiwa sambamba na mwanadada Rachael anaetamba na wimbo wake wa Ole temba,kwa pamoja wakilishambulia jukwaa la Fiesta usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,atambulikae kwa jina la kisanii Ommy Dimpo akiwaimbisha mashabiki wimbo wake wa nani kama mamaa, kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage
Sehemu ya umati wa watu wakishangweka na Fiesta .
Mmoja wa wakali wa kukamua mangona kutoka Clouds FM,Dj Zero akikamua  ngoma jukwaani mbele ya umati wa wakazi wa Shinyanga kwenye tamasha la Fiesta ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage
Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage,wakishuhudia tamasha la Fiesta 2014 likifanyika.
Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa ndani ya uwanja mdogo wa Kambarage,wakishuhudia tamasha la Fiesta 2014 likifanyika.
PICHA ZOTE NA MICHUZIJR.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.