ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 11, 2014

TOUCH FOUNDATION KUENDELEA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA TANZANIA

Rais wa Touch Foundation,  Bw. Lowell Bryan akiwa  katika picha ya pamoja na  Balozi Tuvako  Manongi,  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania  Umoja wa Mataifa na Mke wa Balozi, Bibi Upendo Manongi wakati wa  Hafla ya Asante Supper 2014 iliyofanyika  mwishoni mwa wiki,  hafla  hiyo ilikuwa ni kuadhimisha miaka 10 ya Taasisi hiyo  iliyokwenda sambamba na  harambee ya kuchangia  uimarishaji wa sekta ya Afya nchini Tanzania. Touch Foundation inafanya kazi kwa karibu  na  Serikali ya Tanzania na Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki cha Afya na Sayansi Mwambata ( CUHAS)  Bugando Tanzania.   Katika  hafla hiyo, ambayo ilihudhuriwa na   Viongozi wa  CUHAS wakiongozwa na  Mhashamu Askofu Mkuu,  Yuda Thaddaaeus  Ruwa'ichi, Bw. Bryan alisifu na kupongeza utashi wa Kisiasa na Uongozi wa Mhe. Rais Jakaya  Mrisho Kikwete katika kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wananchi , ushirikiano wake  na kutambua kwake mchango wa sekta binafsi katika  eneo hilo.
Balozi Manongi na   Upendo  Manongi  wakiwa na  Padre  Dkt. Peter Le Jacq wa  Shirika la  Maryknoll ambaye alianza kufanya kazi na Bugando Medical Center katika miaka ya  80  ambaye kwa kushirikiana kwa karibu na  Marehemu  Mhashamu Askofu Aloysius Balina walianza juhudi za  kuyatafutia ufumbuzi  matatizo ya sekta ya afya  hasa upungufu wa  Madaktari. Padre Dkt. Jacq pamoja na rafiki zake  alikuwa chumbuko la Kamati ya Touching Tanzania katika  miaka hiyo ya  80 na hatimaye kuzaliwa kwa Touch Foundation mwaka 2004. Dkt. Jacq naye kwa upande wake amesifu na kutambua  mchango wa Mhe. Rais Jakaya Kikwete na kujituma kwake kuimarisha sekta ya afya kwa kushirikiana na wadau wengine.
Makamu Mkuu wa  CUHAS  Professa  Jacob Mtabaji kushoto kwa  Balozi Manongi na  Professa Paschalis Rugarabamu ambao walikuwa sehemu ya Ujumbe  uliohudhuria Asante Supper 2014 wakiwa katika picha ya pamoja na  baadhi ya Maofisa wa  Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
TOUCH FOUNDATION  KUENDELEA KUSAIDIA SEKTA YA AFYA TANZANIA
Na Mwandishi Maalum
Touch Foundation ,Taasisi isiyo ya kiserikali na yenye makao yake nchini Marekani,  mwishoni mwa wiki ( Mei 8),  imeadhimisha miaka kumi ya kazi zake na kuahidi kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzaniana Taasisi nyingine katika uboreshaji na uimarishaji wa sekta ya afya nchini.

Katika hafla iliyojulikana kama   Asante  Supper 2014,  ilihusisha pia utoaji wa tuzo kwa wadau mbalimbali ambao wamekuwa nguzo muhimu ya Taasisi hiyo. Asante Supper  ilihusisha pia harambee ya uchangishaji wa fedha kwa ajili ya kusaidia sekta hiyo ya afya. Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa  Morgan Library Museum, Jijini New York.

Akiwakaribisha wageni waalikwa,  Rais wa Touch Foundation,  Lowell Bryan pamoja na kuelezea mafanikio ya taasisi yake iliyoanzishwa mwaka 2004 katika uboreshaji wa sekta ya afya nchini Tanzania, amewataka wafadhili mbalimbali kuendelea kujitolea na kuchangia zaidi ili sekta ya afya nchini Tanzania iweze kuimarika na hatimaye kumaliza au kupunguza changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo.

Akasema utashi wa kisiasa na wa kiuongozi ambao Mh.Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameonyesha katika, situ kutambuana kuthamini mchango wa Touch Foundation na Taasisi nyigine kama hiyo, bali pia amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba sekta ya afya inaimarika nchini Tanzania na huduma za afya zinawafikia wananchi kule walipo.

Naye Padre Dkt. Peter le Jacq ambaye naye amekuwa na mchango mkubwa wa uimarishaji wa sekta ya afya nchini kupitia Hopistali ya   Bugando anaambaye haswa ni chimbuko la Touch Foundation,  hakusita kutoa shukrani zake kwa Rais Kikwete na kumuelezea kama kiongozi anaye jituma,  kujitolea na mwenye ushirikiano mzuri za sekta binafsi.

Katika Miaka kumi ya uhai wake Touch Foundation imekuwa ikishirikiana na kufanya kazi kwa Karibu na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, na hususani Chuo Kikuu  cha Kikatoliki cha  Afya na Sayansi Mwambata  cha Bugando (CUHAS). 

Ushirikiano huo unahusisha katika maeneo mbalimbali mtambuka yakiwamo mafunzo ya madaktari na wataalam wa fani mbalimbali kupitia CUHAS na hivyo kuchagia ongezeko la madaktari na wataalam.

Mbali ya watendaji wakuu wa  Touch Foundation,  wakiongozwa na Rais wake, Bw. Lowell Bryan, pamoja na wafadhili. Asante Supper 2014 ilihudhuriwa pia na wageni maalum kutoka Tanzania na ujumbe huo ulihusisha Muhashamu Thaddaeus Ruwa’ichi Askofu Mkuu wa Mwanzana Mwakilishiwa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi alikuwa miongoni wa wageni waaalikwa.

Wengine kutoka  CUHAS walikuwa ni Askofu Augustine Shao,   Makamu Mkuu wa  CUHAS , Profesa Jacob Mtabaji,  Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine,  Padre Dkt. Charles Kitima, Profesa Paschalis Rugarabamu, Dkt, IsidorNyahomela, Dkt. Frederick Kigadye, Dkt. Charles Majinge,  Dkt. Manage Manyama, Dkt. Stella Mongella,  Dkt. Godwin, Godfrey Sharauna Sister Marie- Jose Voeten kutoka hospitali Teule ya Sengerema.

Baadhi ya Madaktari hao kutoka Bugando na hasa wale walio nufaika na ufadhili wa Touch Foundation walielezea walivyo nufaika na ufadhili huo ambao umewawezesha kusoma, kujipatia ujuzi na hivyo kupata fursa ya kuwahudumia watanzania wenzao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.