ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 21, 2014

MVUA NI NEEMA LAKINI TUSIPO JIPANGA MATOKEO YAKE.....

Barabara ya Lumumba jijini Mwanza na heka heka zake katika kipindi cha mvua.
Mifereji ya maji taka ni finyu nayo ikishinda bila kufanyiwa usafi ikiwa ni pamoja na uzibuaji hali huwa tete.
Adha waipatayo wafanyabiashara waliopangisha kwenye maduka ya majengo yaliyopo pembezoni kwa kituo cha daladala za Mwaloni zamani karibu na soko kuu.
Mitaro imejaa, barabara zimejaa maji, Si biashara tena bali sasa ni kila mmoja kuokoa mali zake.
Chepe chepe...dugu yake tepe tepe.
Ili kuepuka kadhia hii ambayo kama mvua ingenyesha nyakati za usiku ingekuwa hasara kubwa kwa mali zilizowekwa sakafuni, basi ni jukumu sasa la kila mfanyabiashara kuhakikisha takataka za maboski, mifuko, vitambaa na bidhaa nyingine za kutupa, kuwa zinahifadhiwa kwenye mapipa maalum ya taka na si kuyaelekeza kwenye mifereji ya maji taka.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.