ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, September 29, 2013

SERENGETI FIESTA 2013 MWANZA NOWMA...!

Anaitwa Neylee,msanii wa bongofleva ambaye kwa sasa anafanya vyema sana kwenye anga ya muziki huo,akiimba kwa hisia mbele ya mashabiki wake usiku wa kuamkia leo wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea 2013.

sehemu ya mashabiki wakifuatilia yanayojiri ndani ya uwanja wa ccm kirumba,ambapo tamasha la serengeti fiesta likirindima .
Msanii wabongofleva akicheza na shabiki wake jukwaani .
Mashabiki wakishangweka kwa raha zao huku jukwaala fiesta likiwaka moto vilivyo .
Kundi la Wasanii mahiri wa kuimba na kucheza kutoka THT,wajiitao Makomanda wakitumbuiza  ndani ya uwanja wa CCM Kirumba,ambapo tamasha la Serengeti fiesta 2013 likiendelea.
Muigizaji wa filamu lakini pia ni msanii wa muziki wa kizazi kipya,aitwaye kwa jina la kisanii Shilole akiimba mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa ccm kirumba .
Anaitwa Christian Bella ambaye alikuwa akifanya vyema sana kwenye bendi ya muziki wa dansi ya Acudo,akiwaimbisha mashabiki wake  ndani ya tamasha la serengeti fiesta 2013.
Mkali mwingine wa hip hop,ambaye amekuwa akifanya vyema sana kwenye anga hizo,Kalla Jeramiah akishusha mistari mikavu mbele ya mashabiki wake .

Wako live kinoma ,huku mayowe na miluzi ikiwa imetawala kila kona ya uwanja
Pichani kati ni Meneja Mawasiliano wa kampuni ya simu za mikononi ya Zantel akiwa na marafiki zake wakilifuatilia tamasha la serengeti fiesta 2013  ndani ya uwanja wa ccm kirumba,ambapo wakazi wa jiji la Mwanza wamejitokeza kwa wingi.
Kila kona ni ileee full maraha tuu,huku wakiburudika na vunywaji mbalimbali kutoka kampuni ya bia ya Serengeti ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha la serengeti fiesta wakishirikiana na PSI kupitia bidhaa yao ya Salama kondom.
Vijana machachari kabisa kutoka kinondoni wakitambulika kwa jina la KINOKO wakionesha umahiri wao wa kucheza ngoma za Michael Jackson mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza.
Mmoja wa sanii waliofanya vyema sana katika shindano la BSS,Walter Chilambo,akiimba kwenye jukwaa la Serengeti fiesta.
Mashabiki wa fiesta kibao usiku wa kuamkia leo ndani ya ccm kirumba.
Vuta rahaa hakuna maneeeee.....manenooooo
Mtangazaji wa Clouds Paul James na wadau wake wakifuatilia yanayojiri ndani ya tamasha la serengeti fiesta  ndani ya ccm kirumba.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.