ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 22, 2013

MSHINDI WA NYUMBA WA AIRTEL YATOSHA ATEMBELEA NYUMBA YAKE

Mkurugenzi wa kitengo cha mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya akikata utepe na familia ya Mshindi wa nyumba wa promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba  bwana Silvanus Juma (wa kwanza kushoto) wakati wa makabithiano ya nyumba yalifanyika kigamboni jijini Dar es Saalam

Mshindi wa nyumba wa promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba  bwana Silvanus Juma pamoja na mke wake wakiingia katika nyumba wakati walipotembelea nyumba kigamboni jijini Dar es saalam

Mkurugenzi wa kitengo cha mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya  akimkaribisha mshindi wa nyumba bwana Silvanus Juma pamoja na familia yake  wakati wa makabithiano ya nyumba yalifanyika kigamboni jijini Dar es Saalam

Mkurugenzi wa kitengo cha mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya akimkabithi ufunguo wa nyumba mshindi wa  kwanza wa nyumba ya  promosheni ya Airtel Yatosha shinda nyumba  bwana Silvanus Juma  katika halfa makabithiano iliyofanyika kigamboni jijini Dar es Saalam, akishuhudia ni mke wa mshindi wa nyumba

Mshindi wa nyumba wa promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba  bwana Silvanus Juma akifurahia ushindi na mama yake mzazi mara baada ya kutembelea nyumba kigamboni jijini Dar es salaam


Mshindi wa Nyumba wa Airtel Yatosha Atembelea nyumba yake
  • Makabidhiano hayo yalifanywa mbele ya Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
  • Zaidi ya shilingi milioni 45 na Nyumba mbili bado kushindaniwa
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imemkabithi mshindi wa nyumba mkazi wa Iringa bwana Silvanus Juma Nyumba ya kisasa ya vyumba zitatu yenye thamani ya shilingi milioni 65  baada ya kuibuka mshindi katika wa droo ya kwanza ya mwenzi ya promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba iliyofanyika tarehe 5th August 2013.

Akionge wakati wa halfa ya makabithiano mshindi wa nyumba Bw Silvanus Juma alisema” nimefurahi sana kushinda zawadi hii ya nyumba kutoka Airtel. Mipango yangu na Ndoto yangu siku zote imekuwa nikumiliki nyumba na leo kupitia promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba Airtel imeniwezesha kufanya ndoto yangu kuwa kweli kwa kushinda nyumba hii ya kisasa. Napenda kuwashukuru sana Airtel kwa zawadi hii kubwa ambayo mimi na familia yangu tutaifurahia siku zote. Nawahimiza watanzania wenzangu na wateja wa Airtel wajiunge na huduma ya vifurushi vya Airtel yatosha na kupata nafasi ya kushinda kama mimi”

Akiongea wakati wa makabithiano Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya alisema”  lengo letu wakati tunazindua promosheni hii ni kuona maisha ya watanzania yanabadilika na tayari tunaona na kuthibitisha haya. Silvanus Juma amejishindia nyumba ya kisasa ya vyumba vitatu iliyopo kigamboni jijini Dar es salaam kwa kushiriki kwenye promosheni ya Airtel yatosha na kununua vifurushi na kutumia huduma yetu ya Airtel yatosha.  bado tunazo nyumba 2 kushindaniwa,  ni rahisi sana kushiriki piga *149*99# kisha ujiunge kwenye vifurushi vya Airtel yatosha na upate nafasi ya kushinda shilingi millioni moja kila siku au nyumba mwisho wa mwezi.

Mallya aliongeza kwa kusema” Airtel bado itaendelea kuwazawadia wateja wake kupitia promosheni ambazo zitaleta mabadiliko katika maisha yao na kuendelea kuthibitisha kwa hakika  kuwa Airtel Yatosha”

Promosheni ya Airtel yatosha bado inaendelea mpaka sasa jumla ya shilingi million 44 na nyumba zimeshatolewa kwa wateja katika maeneo mbalimbali nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.