ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, May 21, 2013

LEO NI MIAKA 17 TANGU AJALI YA MV BUKOBA NI TAREHE SAWA NA SIKU ALIYOZALIWA KALA JEREMIAH

Siku hii yenye historia ya majonzi yaani Tarehe 12 mwezi May vilevile ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa msanii anayewania tuzo za Kili 2013, Kala Jeremia (Pichani), yeye katika siku hii huwa aisherehekei bali  hutenge muda kwa sala na maombi

Tarehe 21/may/2013 Tanzania imeadhimisha miaka 17 tangu meli ya MV BUKOBA kuzama ndani ya ziwa Victoria na kusababisha taifa kupoteza raslimali watu ambapo zaidi ni ya watu ELFUMOJA wanatajwa kufa maji kwenye ajali hiyo iliyoiletea simanzi kubwa taifa la Tanzania.
Hivi karibuni wasanii wazawa wa jiji la Mwanza walio nyumbani na wale walio mikoa ya mbali walirejea nyumbani na kujumuika na wenzao kufanya usafi kwenye makaburi ya watu waliofariki dunia kwenye ajali ya Mv. Bukoba kama sehemu ya shughuli za jamii. Pichani ni H.Baba na Mwanachemba Squard Dark Master.

Wananchi wa kanda ya ziwa leo wanajumuika pamoja na marafiki waliopoteza ndugu na jamaa zao katika makaburi hayo maalum ya marehemu hao yaliyoko eneo la Igoma jijini Mwanza kwa ajili ya Ibada ya kumbukumbu. 

Mwenyezi mungu ndiye mpangaji wa yote, jina lake lihimidiwe.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.