ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 3, 2013

AIRTEL YATANGAZA MSHINDI WA MILLION 50 WA PROMOSHENI YA AMKA MILLIONEA


Mwandishi wa Clouds TV Austin Bayadi ( wakwanza kushoto) akibonyesha kitufe cha komputa wakati wa droo kubwa ya mwisho ya kumtafuta mshindi wa shilingi million 50 wa promosheni ya Amka millionea ambapo bwana Layakal Akbar Thawer mkazi wa Dar es salaam aliibuka mshindi wa promotion hiyo. Wakishuhudia ni meneja uhusiano wa Airtel  Jackson Mmbando(aliyekaa katikati) akifatiwa na mwakilishi wa bodi ya michezo ya Bahati Nasibu Emmanuel Ndaki akifatiwa na Afisa masoko wa Airtel  Khalila Mbowe


Meneja Uhusiano wa Airtel  Jackson Mmbando(katikati) na Afisa masoko wa Airtel  Khalila Mbowe kwa pamoja wakionyesha droo ya kumtafuta mshindi wa millioni 50 wa Amka millionea inavyotafuta mshindi wakati wa droo hiyo iliyofanyika katika makao makuu ya Airtel Moroco na kushuhudiwa na Waandishi wa habari, akishuhudia kulia ni mwakilishi wa bodi ya michezo ya Bahati Nasibu Emmanuel Ndaki


Meneja Uhusiano wa Airtel  Jackson Mmbando(aliyekaa katikati) akiongea na wandishi wa habari (hapo pichani) wakati wa droo kubwa ya mwisho ya kumtafuta mshindi wa shilingi million 50 wa promosheni ya Amka millionea ambapo bwana Layakal Akbar Thawer mkazi wa Dar es salaam aliibuka mshindi wa promosheni hiyo.  Kushoto ni mshindi wa million 15  wa promosheni ya Amka milionea bwana Juma Ibrahim Hiza mkazi wa Dar es Saalam na kulia ni  mshindi mwingine wa shilingi milioni 15 Bwana  Adnan Ayub Khan mfanyabiashara  Simiyu.



Airtel yatangaza mshindi wa million 50 wa promosheni ya Amka millionea
·         Zaidi ya washindi 1458 wazawadiwa pesa taslimu zenye thamaniya shilingi million 626 Hadi mwisho wa promosheni hii
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imechezesha droo ya mwisho ya promosheni ya Amka millionea na kumzawadia mshindi  wa droo hiyo kitita cha shilingi million 50.

Droo hiyo kubwa na ya mwisho ilifanyika katika makao makuu ya Airtel morocco na kushuhudia na waandishi wa habari ambapo mkazi wa Kariakoo Dar es Salaam  Bwana Layakal Akbar Thawer  mwenye umri wa 60  mafanyabiashara wa duka la rangi aliibuka kuwa mshindi wa millioni 50 na kutangazwa rasmi kuwa mshindi.

Akiongea wakati wa droo hiyo, Mkuu wa kitengo cha Masoko wa Airtel Levi Nyakundi alisema,  Mpaka sasa Airtel kwa kupitia promosheni ya Amka millionea imewazawadia watanzania na wateja wengi nchini. leo tunashuhudia bwana Akbar akiibuka kuwa mshindi wa pesa taslimu shilingi million 50 kupitia promosheni hii ya Amka millionea na Airtel. 

Hii inathibitisha thamira yetu ya kutuoa huduma bora na bei nafuu huku tukiendelea kuwazawadia watanzania na wateja wetu kwa kupitia promosheni mbalimbali ikiwemo hii ya Amka millionea
Tunaahiidi kuendelea kuboresha huduma zetu na kuhakikisha tunawafikia watanzania wengi zaidi,  mpaka sasa kwa kupitia huduma ya Airtel yatosha wengi wamepata unafuu wa gharama za mawasiliano na kuwezeshwa kupiga simu kwenda mitandao yote nchini na kushuhudia kuwa kweli Airtel yatosha. 

Tunaamini kwa kuendelea kuongeza ubunifu katika huduma zetu na  kuwazawadia wateja wetu kwa kupitia promosheni mbalimbali pamoja na huduma bora zikiwemo za kibenki kupitia Airtel money na huduma ya internet ya kasi zaidi ya 3.75G wateja wataendelea kupata suluhusho la mawasiliano na za kimtandao zilizo bora , za uhakika na gharama nafuu aliongeza Nyakundi.

Akiongea kwa njia ya simu mshindi wa shilling million 50 bwana Layakal Akbar Thawer alisema “ mimi nimekuwa mteja wa Airtel kwa miaka 7 sasa na nafurahia huduma zao, napenda kuwambia watanzania washiriki promosheni hizi nao wananafasi ya kuibuka washindi. 

Promosheni ya  Amka milionea ilizinduliwa rasmi mwenzi December mwaka jana na kuongezewa muda wake mwenzi machi mwaka huu, mpaka sasa wateja zaidi ya1458 na pesa taslimu zenye thamani ya zaidi ya shilingi  million 626 zimezawadiwa kwa washindi walioibuka kutoka katika mikoa mbalimbali nchini.

Mshindi mwingine wa shilingi million 50 alipatikana na kuzawadia mwenzi watatu naye ni Mwalimu wa shule ya msingi na mkazi wa manyara kiteto bwana Grayson Safieli Kabora , huku washindi wa shilingi million 15 wakiwa ni pamoja na  Juma Ibrahim Hamza  umri wa miaka 30 na mkazi wa kawe  Dar es Saalam na Adrian Ayub khan umri wa miaka 25 mfanyabiashara Simiyu

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.