ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 17, 2013

KWA HERI BI KIDUDE.

Mwimbaji mkongwe wa taarab asilia na muziki mahadhi ya pwani ya Zanzibar nchini Tanzania Fatma Bin Baraka maarufu kama Bi Kidude amefariki dunia.

Akiongea kutoka Zanzibar mjukuu wa marehemu ambaye naye anaitwa Fatma Kidude amesema kuwa bibi yake amefariki akiwa nyumbani kwa mtoto wa kaka yake maeneo ya Bububu mjini Zanzibar.

Fatma ambaye naye pia ni mwimbaji wa kundi la Gusa Gusa la jijini Dar es salaam amesema kuwa bado taratibu zote za mazishi zinaendelea kufanyika lakini mwili wa marehemu utahamishwa kuelekea nyumbani kwake Raha leo.

Mara kadhaa kulitokea uzushi wa Bi Kidude kufariki na baadaye kukanushwa, lakini safari hii taarifa hizi ni sahisi kwani zimethibitishwa.

Mwenyezi Mungu ailaze pema peponi roho ya marehemu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.