ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 18, 2013

H. BABA AINGIZA SOKONI PIPI ZENYE JINA LAKE


H. Baba akionesha pipi zake.

Katika kuonyesha kwamba bado ana kiu ya kuona sanaa yake inakuwa na kuvuma mbali huku akiboresha maisha yake, kukuza kipato na kuongeza ufanisi wa kikazi, msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini H. Baba ameamua kujikita katika biashara kwa style ya kiutofauti kwa kuingiza sokoni bidhaa aina ya pipi zenye jina, picha na chata zake, pipi zinazojulikana kwa jina la 'H. BABA & FLORA MAPENZI KWA WATOTO'.

Muonekano wa mbele.
Pipi hizo zilizapambwa kwa picha ya H. Baba katika karatasi ya kuishika pipi, zikipambwa na mfuko wa nylon wenye uzito wa gram 250 uliona picha ya mwanamuziki H. Baba na mwigizaji wa Bongo movie Flora Mvungi, zinazo tengenezwa na kampuni ya TANFRIK LIMITED ya Nairobi nchini Kenya, tayari zimeanza kuuzwa kwenye baadhi ya maduka na vibanda mbalimbali vya biashara kanda ya ziwa.
Muonekano wa nyuma.

Blogu hii imekutana naye uso kwa uso jijini Mwanza akiwa na mzigo wa pipi hizo na swali la kwanza kwake lilikuwa kipi kimepelekea kwa msanii H. Baba kuja na ubunifu huo ambao ni wa kwanza kabisa nchini Tanzania?..... (BOFYA PLAY KUSIKIA JIBU )


Msanii Lady Jay Dee miaka michache liyopita alikuja na bidhaa za maji zenye jina lake, mzigo ukaingia sokoni kisha baada ya muda mzigo ukatoweka sokoni, unawathibitishia vipi wateja kuwa pipi za H. Baba zitadumu sokoni? ......(BOFYA PLAY KUSIKIA JIBU)

"Lete mzigo tuonje!!" Hivi ndivyo wanavyoonekana kusema kutoka kushoto ni mtangazaji wa Passion Fm ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mwanza Kwanza Philbert kabago, H. Baba (mgawa pipi), Samadu Abdul wa Clouds Fm 88.1 Mwanza na Tecnix Muheshimiwa.
Sasa ni zamu ya wadau wa Metro Fm kufurahia utamu Loyce Nhaluke, Sefroza Joseph, Smith King Presenter and Amina Rashidi.

Kwa uwekezaji huu kwenye pipi za H. Baba ndiyo tuseme kuwa hili sasa ni hitimisho kwako kujishughulisha na sanaa ya muziki?.... (BOFYA PLAY KUSIKIA JIBU)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.