ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 13, 2013

MKUTANO WA TATU WA WADAU WA NSSF WAANZA RASMI LEO JIJINI ARUSHA

Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Gaudencia Kabaka akizungumza na kuzindua wimbo maalum wa NSSF uliotungwa na Wasanii hapa nchini wajiitao All Stars,mbele ya wadau waliohudhuria mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.Kauli mbiu ya mkutano huo kwa mwaka huu ni Sekta ya hifadhi ya Jamii Tanzania,Njia panda-Nini kifanyike.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau akifafanua jambo kwa umakini  mbele ya  Wadau zaidi ya 1000 kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya Tanzania, kwenye mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) unaondelea hivi sasa kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha,ambapo kauli mbiu yake kwa mwaka huu ni Sekta ya hifadhi ya Jamii Tanzania,Njia panda-Nini kifanyike..
  
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crenscentius Magori akifafanua jambo mapema leo asubuhi wakati mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,ukiendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Meneja wa kanda na anaeshughulikia Idara mbalimbali za serikali kutoka NSSF,Rehema Chuma akifafanua namna ya uendeshaji wa shirika hilo kwa  wadau waliohudhuria mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe akichangia moja ya mada zilizokuwa sikitolewa kwenye mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Wakili Harold Sungusia akichangia moja ya mada zilizokuwa sikitolewa kwenye mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulioanza leo Februari 13,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Mmoja wa wajumbe wa NSSF,Peter Sumbi aliyekuwa akifanya kazi shirika la Wildlife Fund akitoa ushuhuda wake,namna alivyopata ajali na kufanikiwa kupata fao lake la ajali kazini kutoka kwa shirika la NSSF na hatimaye kufaidi matunda kupitia mfuko huo.
Pichani ni Mwenyekiti wa wasataafu wa TAZARA,Injinia Mwl.Sango akitoa ushuhuda wake kuhusiana na namna shirika la NSSF lilivyowasaidia wastaafu wa shirika la TAZARA,kupitia mfuko wa pensheni na fao la kujitoa.

Sehemu ya Meza kuu ya mkutano huo.

Sehemu ya Wabunge waliopo kwenye mkutano huo.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Mifuko ya Jamii nchini wakiwa kwenye mkutano huo.

Baadhi ya watendaji wakuu wa NSSF wakiwa mkutanoni.

Meneja Mahusiano wa PPF,Lulu Mengele na  Meneja Mahusiano wa SSRA,Sarah Kibonde wakifuatilia yanayojiri ndani ya mkutano huo unaoendelea hivi sasa.
Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini (CHADEMA),Mh Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu akiwa sambamba na Mbunge wa Arumeru Mashariki,Mh Joshua Nasari (CHADEMA) na Wadau wengine wakifuatilia yanayojiri hivi sana kwenye mkutano wa NSSF.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali wakifuatilia yanayojiri ndani ya mkutano wa NSS unaoendelea hivi sana ndani ya ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha.

Mbunge wa jimbo la Ludewa,Mkoani  Njombe,Mh. Deo Filikunjombe (CCM) akiwa na baadhi ya Wabunge Wenzake wanaohudhuria mkutano huo wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijiri ndani ya mkutano huo ambao umewakutanisha wadau zaidi ya 1000 kutoka sehemu mbalimbali jijini Arusha.
Mwenyekiti wa kikao cha awamu ya kwanza cha Mkutano wa tatu wa Wadau wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Bwa.Daudi Msangi akitoa utaratibu kwa Wanachama na wadau mbalimbali waliohudhuria mkutano huo unaoendelea ,kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC,jijini Arusha,kulia kwake ni  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),Dkt. Ramadhan Dau akizungumza jambo na  Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Crenscentius Magori mapema leo asubuhi kabla ya kuanza kwa mkutano wa shirika hilo.
Wadau.

Wadau.

Mkutano ukiendelea.
  

Picha zote na Othman Michuzi

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.