ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 12, 2013

SERIKALI INATEGEMEA KUONA MABADILIKO YA KIMAENDELEO KWA WAFUGAJI: ASEMA MKUU WA WILAYA YA MAGU.

Mkuu wa wilaya ya Magu Jaquelline Liana akifunga Warsha ya siku tatu kwa mafunzo ya Ufugaji Bora kwa wafugaji wa kata za Kahangala Na Nyigogo wilayani humo, mafunzo yakidhaminiwa na Kampuni mpya ya usindikaji nyama iliyoamua kuwekeza wilayani humo ya Alpha Choice LTD .


Nae Mkurugenzi wa wilaya ya Magu Mwl. Naomi Nnko ameushukuru uongozi wa Alpha Choice LTD kwa kudhamini utolewaji mafunzohayo kwani kupitia mafunzo hayo si kwamba wafugajihaowatapata elimu bali pia kutaongeza mahusiaano na ukuzwajiwa pato la Halmashauri ya wilaya kwa maslahi ya uchumi wa Taifa.


Bi. Mary Mashulano ambaye ni Afisa Mifugo upande wa ukaguzi wa nyama akiwaonyesha wafugaji moja ya vifaa maalum vya kukatia pembe na kwato wakati wa warsha ya siku tatu ya elimu kwa wafugaji iliyofanyika katika kata ya Kahangara wilayani Magu mkoani Mwanza.


Mmoja wa wafugaji akiuliza swali ili kupata ufafanuzi juu ya matumizi ya zana zilizoonyeshwa kupitia warsha ya siku tatu ya wafugaji iliyomalizika jana wilayani Magu , ikishirikisha wafugaji wa vijiji vya Bugabu na Kahangara vilivyo katika kata ya Kahangara na kijiji cha Ilungu kilichopo katika kata ya Nyigogo.


Wafugaji wakijadiliana na kunakili masualamuhimu ya kuzingatia.


Bi. Mary Mashulano ambaye ni Afisa Mifugo upande wa ukaguzi wa nyama akitoa darasa kwa wafugaji juu ya kanuni zilizo bora katika kuhudumia wanyamakupitia warsha ya siku tatu ya wafugaji iliyomalizika kwa mafanikio makubwa jana wilayani Magu, ikidhaminiwa na Kampuni mpya ya Usindikaji nyama ya Alpha Choice, ikishirikisha wafugaji wa vijiji vya Bugabu na Kahangara vilivyo katika kata ya Kahangara na kijiji cha Ilungu kilichopo katika kata ya Nyigogo .


Mtaalamu kutoka Halamashauri ya wilaya ya Magu akikokotoa hasara za matumizi mabaya ya dawa za kutibu na kujikinga maradhi kwa wanyama wafugwao, katika warsha ya siku tatu ya elimu kwa wafugaji iliyofanyika katika kata ya Kahangara wilayani Magu mkoani Mwanza.


Maelekezo ya matumizi halisiya dawa yalitolewa na wataalamu hao.


Picha ya pamoja kwa viongozi na wana warsha wa mafunzo ya Ufugaji Bora kwa wafugaji wa kata za Kahangala Na Nyigogo wilayani humo, mafunzo yakidhaminiwa na Kampuni mpya ya usindikaji nyama iliyoamua kuwekeza wilayani humo ya Alpha Choice LTD ..

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.