ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 31, 2012

DIWANI ILALA ATEMBELEA KAMBI YA MISS UTALII WILAYA NA KINONDONI

 Mh. Ghalib Riyami akiwaasa jambo washiriki miss Utalii.

Mh. Ghalib Riyami na picha ya pamoja na washiriki hao.

MHESHIMIWA DIWANI ILALA ATEMBELEA KAMBI YA
MISS UTALII ILALA NA KINONDONI
Diwani wa kata ya mchikichini na mwenyekiti  wa madiwani wa kata tano (ilala, mchikichini, kariakoo,gerezani na jangwani)  mheshimiwa Ghalib Riyami ametembelea kambi ya washiriki wa Miss Utalii wilaya ya Ilala 2012 na Miss Utalii Wilaya ya Kinondoni2012 Kambi hiyo ya pamoja kati ya warembo wanao wania taji la Miss Utalii Ilala 2012 na wale wanao wania taji la Miss Utalii Kinondoni 2012 ipo katika Hoteli ya kitalii ya Nyota 3 ya Lamada Hotel.

Mheshimiwa diwani ameelezea kufurahishwa kwake kwa wilaya ya Ilala kupewa heshima ya kuwa wenyeji wa shindano hilo la kihistoria ambapo wilaya mbili kwa pamoja zinashindana kuwania mataji ya wilaya zao katika ukumbi na steji moja tena siku moja. “Najua waandaaji wangeweza kuamua shindano hili lifanyikie kinondoni,lakini mmeamua kutupa heshima hiyo sisi wa wilaya ya ilala,hakika tumefarijika sana” Aidha katika kuonyesha furaha yake na kupokea heshima hiyo aliyo iita kubwa Mheshimiwa diwani aliahidi kuwa yeye binafsi pamoja na madiwani wa wilaya ya ilala watahakikisha wanasaidia na kuunga mkono kwa hali na mali kufanikisha kufanyika kwa shindano hilo,kama lilivyopangwa yaani tarehe 14/09/2012 katika hotel ya Lamada.

Aliwataka warembo wanaoshiriki shindano hilo kutambua kuwa shindano hili tofauti na mashindano mengine ni alama ya urithi wa Taifa na kielelezo cha utamaduni wa mtanzania,hivyo wanapaswa kutambua kuwa na nidhamu na kuvaa uhalisia wa mtanzania siku zote na wakati wote mashindanoni nan je ya mashindano.

Amewakumbusha na kuwaomba kutumia shindano hili kutangaza utalii wa Wilaya ya ilala na mkoa kwa ujumla ikiwemo UWANJA WA NDEGE WA Juliasi Nyerere,Soko la kariakoo,makumbusho ya taifa,sokola kimataifa la samaki la magogoni,shule ya Pugu ambayo mwalimu Nyerere alifundisha, na ufukwe wa bahari ya hindi.

Mheshimiwa diwani aliwashukuru na kuwapongeza wadhamini mbalimbali ambao wamethibitisha kudhamini shindano hili,wakiwemo Lamada |hotel,105 Times FM Radio,Kahama Gold Mine,Traventine Hotel,Mzee Yusuph Enterprises,Easy Media,Daja Saloon,Zizu Fashion,Tambaza Cort Brocker and Action Mart,Dagaa Finance na Aucland Travel and Tours,Hameed Designer.Gabriel Designer  Ametoa wito kwa makampuni na watu mbalimbali kudhamini na kuchangia shindano hili ambalo gharama za kuandaa ni kubwa hivyo kuhitaji mchango wa hali na mali.

Jumla ya warembo ishirini na nne(24)kumi mbili kutoka wilaya ya kinondoni na kumi na mbili kutoka wilaya ya Ilala kwa pamoja watachuana ili kupata taji la miss utalii wa wilaya ya Ilala na  miss utalii wilaya ya kinondoni.Wilaya ya Ilala washiriki ni; Zourha Malisa, Nancy Musheruzi, Princess Lemi, caroline Yust, Eunice George, Naomi Michael, Lucy Julius, Nurina Mikindo, Rose James, Salome Kiula, Marry Wambura na Judith Frank. Wahiriki wa wilaya ya Kinondoni ni; Mwasiti Thabit, Irene Richard, Hellen Herman, Fatma Hussein, Rachel Magai, Neema Mbeju, Neema Ngowi, Duda Tumbo, Zahra Waziri, Janeth  Nelson, Teddy Paul na Ruby Kivunjo.

Akizungumza na warembo hao muheshimiwa diwani alisisita umuhimu wa warembo hawa kulitumikia taifa kwa kutangaza vivutio vya kitalii kitaifa na kimataifa ili kusaidia kuinua uchumi na kuongezeka kwa pato la taifa wakati huu ambapo sekta ya utalii inachangia asilimia zaidi ya kumi na saba(17%) ya pato la taifa.

Alisisitiza umuhimu wa kuelimisha vijana mashuleni ili kukuza na kuhamasisha utalii wa ndani pia alisisitiza haja ya kutangaza kwa nguvu zote vivutio vya utalii vya nchi yetu ya Tanzania ili kuongeza idadai ya watalii wanaotembelea, ikiwa hadi leo kulingana na takwimu Tanzania hutembelewa na watalii laki nane(800,000) kwa mwaka na hii ni idadi ndogo ukilinganisha na nchi jirani zinazotuzunguka.

Pia alitoa wito kwa wazazi kuondokana na dhana potofu juu ya mashindano ya urembo na aliwaasa mabinti kuwa na heshima, adabu na haiba nzuri ili kuifanya jamii kubadili mtazamo juu ya mashindano haya yenye tija kwa taifa letu kwa kuwa linatangaza utalii wa taifa hili la Tanzania.

Mwisho aliahidi ushirikiano wa hali na mali katika kufanikisha shindano hili ambalo limepangwa kufanyika katika ukumbi wa lamada hotel ambao upo katika umoja wa kata tano anazoziongoza.

Yelemia Myenga
Mkurugenzi Miss Tourism Tanzania Organisation – Ilala na Kinondoni

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.