ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 13, 2012

MALAWI MABINGWA KOMBE LA AFRICA NETIBOLI

Mabingwa wa michuano hiyo timu ya Malawi wakipiga picha pamoja na mgeni rasmi mama Asha Bilal.
 Timu ya Taifa Queen ikiwa katika picha ya pamoja na kombe lao.
Mke wa Makamu wa Rais Mama Asha Bilal wa nne kutoka kushoto na mama Tunu Pinda wanne kutoka kulia pamoja na wake wa viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja na timu ya taifa ya Netiboli Taifa Queen mara baada ya kukabidhiwa kombe lao la ushindi wa pili katika michuano ya Afrika ya Netiboli, baada ya Malawi kuchukua ubingwa huo, fainali hizo zilifanyika jana kwenye uwanja wa Taifa wa ndani na kufuatiwa na hafla fupi nyumbani kwa Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda.

Hata hivyo fainali hizo zilichelewa kuanza kutokana na hali ya hewa ambapo muda mwingi mvua ilikuwa ikinyesha na kufanya waandaaji kuhamisha uwanja wa kuchezea mara kwa mara kutoka uwanja mkubwa wa Taifa na uwanja wa ndani Shukrani zimwendee mama Tunu Pinda kwani juhudi zake zilizozaa matunda na ni wazi kwamba hata wachezaji wa timu hiyo ya Taifa Queen wamefurahia sana michuano hii na wanajiona kwamba kweli walikuwa wakiwakilisha taifa, lakini pia pongezi ziwaendee watanzania wakiongozwa na mama Tunu Pinda pamoja na kamati yake, Hongera sana mama kwa kutoa zawadi nono kwa wachezaji.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.