ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 20, 2012

CHELSEA MABINGWA UEFA 2012

Ni Chelsea toka nchini Uingereza ndiyo mabingwa wa UEFA 2012 mara baada ya kuifunga nyumbani kwao timu ya Bayern katika hatua ya penati 4-3 mchezo uliochezwa kwenye dimba la Fußball Arena München nchini Ujerumani.

Thomas Müller aliipatia bao Baryen zikiwa zimesalia dakika saba tu mchezo kumalizika haliiliyowafanya wengi kuamini kuwa mchezo utamalizika kwa matokeo hayo hivyo wakali hao wakicheza nyumbani kutawazwa mabingwa kumbe la hasha haikuwa hivyo... Didier Drogba akasawazisha dakika ya 88 kupitia kichwa safi kwa mpira wa kona.

Hadi dakika 90za mchezo zinamalizika timu zote zilitoka sare ya bao 1-1.

Lakini Bayern itabidi wajilaumu kwani walipata penati katika muda wa dakika 30 za nyongeza kwa makosa ya Drogba kumkwatua Franck Ribéry kwenye eneo la hatari, shujaa wa Chelsea langoni Petr Čech kept aliipangua penati ya Arjen Robben hivyo kuitia mikosi. Hadi mwisho Chelsea Mabingwa kwa jumla ya magoli 5-4.
Wachezaji wa Chelsea wakitimka kusherehekea ushindi mara baada ya Didier Drogba kufunga penati muhimu ya mwisho.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.