Mechi kati ya Kombe la FA kati ya Tottenham na Bolton Wanderers ilisimamishwa ghafula baada ya mchezaji wa Bolton, Fabrice Muamba kuzimia ghafula, na kushindwa kuvuta pumzi.Madaktari walijaribu kwa dakika 10 kumfanya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 aweze kupumua, na hilo liliposhindikana, ilimlazimu mwamuzi Howard Webb kusimamisha mchezo wakati ukiwa 1-1 katika dakika ya 41.
Muamba alizaliwa tarehe 6 Aprili mwaka 1988 mjini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, na aliimarika kisoka katika chuo cha vijana wadogo cha Arsenal, na akiiwakilisha England katika mechi mbalimbali, tangu zile za vijana wa miaka 16, hadi zile za wale wa miaka 21. Alijiunga na Birmingham mwaka 2007, na kuhamia Bolton mwaka uliofuata.
Tangu kufikishwa hospitali, hakuna habari zaidi zilizotolewa kuhusiana na hali yake ya afya hadi sasa.
RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA
-
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe.
Mwanaidi Ali Khamis akigawa iftar kwa mmoja ya mtoto anayelelewa katka
Makao ...
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.