ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 12, 2012

AIRTEL YASHEREHEKEA MAPINDUZI KWA KUKABIDHI MSAADA WA BAISKELI 10 VITUO VYA AFYA WILAYANI MISUNGWI

Katika kuadhimisha sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar, Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi Airtel leo imekabidhi msaada wa baiskeli 10 kwa waganga wafawidhi kutoka vituo 10 vya Idara ya Afya wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila (C) akimkabidhi baiskeli Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Mwagiligi kilichopo wilayani humo huku akishuhudiwa na Meneja Biashara wa Kanda ya Ziwa Kampuni ya Airtel bw. Ally Maswanya (R).

Msaada huu wa Baiskeli utawasaidia waganga wakuu wa vituo vya tiba wa vijiji 10 kukabiliana na tatizo la usafiri.

Ally Maswanya
Airtel Tanzania sambamba na kutoa msaada huu wa baiskeli kwa wauguzi pia imeziwezesha shule mbalimbali nchini kwa misaada ya vitabu, madawati na vitendea kazi kadha wa kadha kwa lengo la kurejesha shukurani kwa wananchi na kuisaidia serikali katika harakati zake za maendeleo.

Sehemu ya wauguzi wa Hospitali Kuu Wilaya ya Misungi waliohudhuria makabidhiano hayo.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila (C) akimkabidhi baiskeli Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Kijima, Dr. Marwa Mwita huku akishuhudiwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Taknolojia, Mbunge wa wilaya ya Misungwi Mh. Charles Kitwanga almaarufu 'Mawe Matatu'.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila akimkabidhi baiskeli Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya Igongwa.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila (C) akimkabidhi baiskeli Mussa Shipemba ambaye alimwakilisha mganga mfawidhi Kituo cha Afya Nyamainza.

Msaada wa baiskeli kutoka Airtel kwa kituo cha Buhunda ukikabidhiwa.

Kaimu Mganga mfawidhi wa Idara ya Afya wilaya ya Misungwi Dr. Beichumila Saula akisoma lisala.
"Tunachangamoto mbalimbali zinazotukabili ikiwa ni pamoja na uhaba wa fedha kuendeshea shughuli mbalimbali, Uchache wa watumishi wa kada mbalimbali, Uhaba wa madawa na vifaa tiba, katika bohari ya dawa ya kanda (MSD), Uhaba wa usafiri katika vituo vya tiba, Asante Airtel".

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Bi. Mariam Lugaila
"Kwa niaba ya watu wangu wa Misungwi - Tunawashukuru sana Airtel tukiwasihi ushirikiano usiishie hapa, uendelee kwani bado kuna mahitaji mengi na makampuni mengine yaige mfano huu"

Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Tekinolojia ambaye ni Mbunge wa Misungwi Mh.Charles kitwanga nae akitoa shukurani.

Mh.Charles kitwanga akipata Picha ya pamoja na wauguzi wa Hospitali ya Wilaya Misungwi.

Misungwi Hospital.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.