
Mkuu wa Kikosi cha Doria cha Idara ya Uvuvi mkoani Mwanza, Juma Makongoro pamoja naye Bwana Lukanga ambaye ni Mkuu wa Maabara ya Ubora wa Samaki iliyopo Nyegezi wamethibitisha kukamatwa kwa samaki hao wachanga kwenye gati la kufikishia samaki kiwandani hapo ambapo wanaaminika kuwa walikuwa ni kwaajili ya kuchakatwa.

Taratibu zinafanyika ili kupata kibali kutoka mahakamani kwa ajili ya kugawa samaki hao kwa baadhi ya shule au taasisi zingine ambazo zinahitaji msaada wa chakula kwa vile samaki hao hawana madhara kiafya na kwamba hatua nyingine kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

Mkurugenzi wa Kiwanda cha Vickfish, Murtaza Alloo, amethibitisha samaki hao kukamatwa lakini amesema samaki hao bado walikuwa ni mali ya wakala kwa vile walikuwa hawajapokelewa kiwandani.
Uchunguzi unaonyesha kuwa kwa kipindi ch miaka mitatu iliyapita viwanda vya kusindika minofi ya samaki vilivyoko eneo la Kanda ya Ziwa vimekabiliwa na uhaba wa samaki , hali ambayo imesababisha viwanda mbalimbali kupunguza wafanyakazi.
Samaki wasio ruhusiwa ni wale walio chini ya ukubwa wa sentimita 50.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.