ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 24, 2011

NINI CHANZO CHA KUKITHIRI KWA WIZI VYUMA CHAKAVU?

Miaka ya nyuma Zoezi la ukusanyaji vyuma chakavu vilivyokusanywa na kuuzwa viwandani ili kuyeyushwa na kutengeneza bidhaa nyingine za chuma, zoezi lilianza vizuri tu kwa watu wakukusanya vyuma vidogo vidogo majalalani, vyuma visivyokuwa na kazi kwenye magereji, vilivyotupwa njiani kiufupi ilikuwa ni vyuma ambavyo ni takataka.
Lakini leo hii ngoma imegeuka!! Thamani ya bidhaa ya chuma imekuwa kama madini, wasio na uungwana wanangoa hadi mifuniko ya mashimo ya maji taka, mabomba ya maji, vyuma vya reli, madaraja, mita za maji, miundombinu ya alama za barabarani na sasa wameyageukia mabango....mmmmmh!.. Naskia uswazi wanapitia majiko, wanangoa hadi mageti..

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. sengo namba ya polisi huijui, ungepiga simu polisi haraka iwezekanavyo, kaniudhi sana huyo jamaa

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.