ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 22, 2011

ARUSHA KIDEDEA KATIKA VODACOM MWANZA CYCLE CHALLENGE 2011.

Picha kulia ni mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Kanda ya ziwa Steven Kingu sambamba na mkuu wa udhamini Vodacom Tanzania George Rwehumbiza wakimkabidhi Mshindi wa kwanza wanaume Richard Laizer kutoka Arusha zawadi ya kitita cha shilingi milioni 1.5 baada ya kuwashinda washiriki wengine 400 kwenye mbio za baiskeli za Vodacom Mwanza Cycle challenge iliyomalizika leo jijini Mwanza na kudhaminiwa na Vodacom sambamba na SBL kupitia Malta Guinness na Redio Clouds.

Mshindi wa pili Mindi Mwangi kutoka mkoani Shinyanga aliyekuwa akitumia baiskeli ya kawaida tu hapa akipokea kitita chake.

Mshindi wa kwanza mbio za baiskeli wanawake kilomita 80 Sophia Husein akipokea kitita cha shilingi milioni moja toka kwa wadhamini.

Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Bia ya Serengeti SBL bw. Ephraim Mafuru akikabidhi zawadi kwa Zavalina Abel aliyeshiriki mbio za kilomita 10 zilizomalizikia katika vilima vya Bugando na hafla ya kukabidhi zawadi kufanyika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

Si mnaona jamaniiii!!

Washiriki katika pozi.

Mkurugenzi wa Masoko Kampuni ya Bia ya Serengeti SBL bw. Ephraim Mafuru kwa upande wake ametoa pongezi kwa chama cha baiskeli kanda ya ziwa kwa kazi kubwa ya kufanya mapinduzi kwenye mashindano hayo ya sita, kuyapendezesha na kuwa na mwonekano wa kitaifa zaidi.

Washiriki mbio tofauti katika pozi wakisikiliza yanayojiri.

Mashindano yalikuwa na kila sifa za kuvutia, vuta hisia kilomita 196 kwa baiskeli...Duh!!

Haaooo darajani...

Ajali nazo zimo hapa ziligongana kama baiskeli saba hivi....kisa utelezi wa ganda la ndizi.

Mtu kule baiskeli kule...!!

Pamoja na walume hawa kutumia baiskeli hizi za teknolojia hawakufua dafu... mbele ya washosha ng'ombe wazee wa shy.

Akitumia baiskeli isiyo na teknolojia (mfupa) mzeiya wa Shy akiovateki tena kwenye kilima...

Balaaa mwanawane, mzee mzima huyoooo....

Kulia mtu, kushoto mtu hapa ni kazi tu..

Hapa jeh!!

Kote tambarare, shughuli ilikuwa ni kukimaliza kilele cha Bugando...

"Isiwe tabu sheria si zinaruhusu, kwenye kilima to finito ... naikokota"


Kutoka kushoto ni Bukuku wa blogu maarufu ya Full Shangwe, Brand Manager wa Malta Guinness bw. Maurice Njowoka, Butunga wa TBC, Blogger maarufu Michuzi Jr na G.Sengo.

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. Thе ωгite-up featurеs рrοven beneficial tо mysеlf.
    It’s eхtremеly helpful and you're simply clearly quite experienced of this type. You have got popped my eyes to different thoughts about this kind of matter along with intriguing, notable and reliable content material.
    Here is my site Http://Wiki.Kspu.Karelia.Ru/Index.Php?Title=Участник:MitchellBa

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.