ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 10, 2011

HAPPY BIRTHDAY MUBELWA BANDIO

Salaam kwako ndugu yangu.
Natumai kuwa u-mzima na unaendelea vema na harakati za mapambano ya maisha.. Nami pia.
Sababu pekee ya wewe kupokea UJUMBE HUU BINAFSI siku hii ya leo ni kwa kuwa umekuwa sehemu ya maisha yangu ndani miezi 12 iliyopita ama zaidi. Hivyo ninapo sherehekea siku yangu ya kuzaliwa (Aug 10), napenda kuleta ujumbe huu mfupi wa SHUKRANI ZANGU ZA DHATI kwa namna ulivyoendelea kuwa mmoja wa wale wanaoyafanya maisha yangu kuwa yalivyo sasa. Iwe ni kwa MANENO, MATENDO ama MAWAZO yako.
Nathamini sana uwepo wako na nakuombea mafanikio katika kila lililo jema utendalo ila maisha yako yawe mfano mwema kwa wengine wengi.
Nikumbushe tu kwamba, katika maisha yetu na katika kila jambo tutendalo, "kuna anayetuona kwa mara ya kwanza na / ama mara ya mwisho" na swali ni kuwa TUNAMUACHA NA TASWIRA GANI KUHUSU SISI NA MAISHA YETU?
Unapendwa, Unakumbukwa na UNAOMBEWA MEMA
ASANTE KWA KUWA ULIVYO

http://www.changamotoyetu.blogspot.com/
http://www.youtube.com/user/mutwiba

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.