ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 5, 2011

PRE SEASSON YA TOTO KUELEKEA LIGI KUU.

Casto Mumbala wa Toto (11) akijaribu kumtoka Maxwel Anthony wa Tinsela.
Katika kujiandaa na mikikimikiki ya ligi kuu soka Tanzania bara Wanakisha Mapanda wa jijini Mwanza Toto Africans katika mechi yake ya kirafiki jioni ya leo wameikandamiza bila ya huruma timu ya Tinsela toka wilayani magu bao 4-0.

Katika mchezo huo huo wa nguvu na wakuvutia uliosheheni kosakosa nyingi magoli ya Toto yalifungwa na Casto Mumbala, Emma swita (bao la pili na la tatu) na bao la nne lilitupiwa nyavuni nae Salum Kamana.

Magoli ya Tinsela yamefungwa na Amani kipanya pamoja naye Maxwel Anthony. Kesho jumamosi timu ya Toto itashuka dimbani katika mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Tanzania Soocer Academy ya jijini Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.