ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 7, 2011

WIKI MBILI KABLA YA KUVAANA NA SIMBA, MOTEMA PEMBE YATIMUA KOCHA WAKE.

Uongozi wa klabu ya DC Motema Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo umetangaza kumuachisha kazi kocha wao Mohamed Nashridine Nabi huku wakiwa katika maandalizi na ya mchezo dhidi ya Simba ya Tanzania kwa ya kuwania nafasi ya kushiriki katika raundi ya makundi ya kombe la shirikisho la Africa.DC Motema Pembe
Timu hizo mbili zitakutana katika mchezo wa kwanza wiki ijayo na kurudiana baada ya wiki mbili.

Motema Pembe kwa sasa imekwenda mjini Goma kucheza mechi za kirafiki za kujiandaa kupambana na Simba huku timu hiyo kwa sasa ikifundishwa na aliyekuwa kocha msaidizi Andy Fulila.


Simba Sc.
Uongozi wa DC Motema Pembe umesema umemuachisha kazi kocha huyo raia wa Ubelgiji, kwa sababu alishindwa kufanya kazi na wasaidizi wake, na pia kushindwa kufanya vyema katika ligi ya nyumbani. Motema Pembe ilifungwa na Ndo Mbosco ya Lubumbashi na TP Elima ya Matadi, kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Kocha Nabi ameviambia vyombo vya habari vya mjini Kinshasa kuwa klabu haijamlipa mshahara wake katika kipindi ambacho walikuwa wakijadili suala lake. Amesema amesikitishwa na uongozi wa klabu hiyo, kwa kuwa alikuwa na mipango mizuri ya kuiongoza klabu hiyo hadi fainali ya Kombe la Shirikisho.

Mchezo wa kwanza kati ya DC Motema Pembe na Simba utachezwa jijini Dar Es Salaam.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.