
Katika siku za hivi karibuni serikali imelaumiwa kwa namna walivyokabiliana na maandamano ya upinzani na kusababishwa kulazwa hospitali kwa mwanasiasa wa upinzani, Dk Kizza Besigye pia kumezua shutma kali.
Wakati atakapoapishwa kwa muhula mwengine,Yoweri Museveni atakuwa amejiongezea muda wa kukaa madarakani kwa takriban miaka thelathini na alipoingia madarakani mwaka 1986 alisema tatizo la viongozi wa Afrika ni kukaa kwenye utawala kwa muda mrefu sana. Kwa miaka mingi amefanya juhudi kuijenga upya nchi ya Uganda baada ya nchi hio kuwa kwenye vita na utawala mbaya.
Bado anaungwa mkono na wengi lakini wadadisi wanaona kuendelea kutegemea jeshi kunaweka nchi hiyo katika mazingira magumu. Kiongozi wa upinzani, Dokta Kizza Besigye,bado yuko nchini Kenya baada ya kupata matibabu kufwatia kushambulia kwake na polisi.

Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.