Pamoja na vurugu hizo, serikali mkoani Mwanza imewataka wafanyabiashara hao kuheshimu sheria na kanuni za mipango miji zilizowekwa pia maafikiano yaliyofikiwa baina ya viongozi wao, uongozi wa mkoa na halmashauri ya jiji hilo .
Vurugu hizo zilizodumu kwa zaidi ya saa sita, zilianza saa tatu asubuhi baada ya mgambo wa jiji na askari wa kutuliza ghasia kuwatawanya wafanyabiashara hao katika maeneo ya Makoroboi, Mission na Soko Kuu.
Kutokana na hali hiyo, machinga walijikusanya na kuanza kuvamia maduka, magari kabla ya kuandamana saa 4:38 asubuhi hadi katika jengo la ofisi za Halmashauri ya jiji la Mwanza wakishinikiza kutoondolewa katika maeneo hayo.
Nje ya jengo hilo , waliweka vizuizi vya mawe katika barabara zote zinazoingia jiji na kulazimisha pikipiki na magari yaliyokuwa yakipita kurudi yalikotoka huku wakiwa na chupa za maji ya kunawa kwa ajili ya kujikinga na moshi wa mabomu iwapo polisi wangewafyatulia mabomu ya machozi.
Baada ya mazungumzo hayo, Kandoro aliwaambia machinga kuwa hapingani na sheria na kanuni za mipango miji kwa kuruhusu machinga wafanye biashara katika maeneo waliyoruhusiwa, isipokuwa wafuate masharti waliyopewa katika maeneo ya Makoroboi, Mirongo, Vitunguu Soko Kuu na Mlango Mmoja.
Baada ya kuondoka katika ofisi za halmashauri hiyo, machinga waliingia mitaani tena na kuanza vurugu wakivamia maduka na kuvunja vioo kwa madai kwa wafanyabishara wengine, hawatafanya biashara.
Sambamba na kuvamia maduka, walijiandaa kwenda kuvamia Kituo cha Polisi Pamba kwa lengo la kukichoma moto kwa kutumia matairi ya gari kabla ya polisi waliokuwa doria kuwawahi na kuwadhibiti, ambapo walitupa matairi ya moto katika barabara ya Pamba jirani na kituo hicho.
Tupe maoni yako
hapo ndipo utajua utamu wa serikali na jamii yake full kumwaga damu
ReplyDeletehapo ndipo utajua utamu wa serikali na jamii yake full kumwaga damu
ReplyDeletehapo ndipo utajua utamu wa serikali na jamii yake full kumwaga damu
ReplyDeletehapo ndipo utajua utamu wa serikali na jamii yake full kumwaga damu
ReplyDeletehapo ndipo utajua utamu wa serikali na jamii yake full kumwaga damu
ReplyDelete