
Wamesema kuna watu ambao idadi yao haijajulikana wamekamatwa.

Kundi la wapiganaji la Kisomali la al-Shabab limesema linahusika na mashambulio hayo kwasababu Uganda inaiunga mkono serikali ya Somalia mjini Mogadishu.

Polisi wamesema, ukanda huo ulikutwa kwenye mfuko mweusi kama ule unaotumika kubebea lap-top kwenye klabu ya usiku Jumatatu mchana.
Mfuko huo ulikuwa na milipuko na mabomu.
Mataifa ya watu hao waliokamatwa hayajatajwa lakini maafisa wamesema kichwa kimoja kilichopatikana karibu na eneo moja lilipotokea mlipuko huo kinaonekana kuwa cha Msomali, ambaye huenda alikuwa amejitoa mhanga.
CHANZO CHA HABARI BBC SWAHILI.
Tupe maoni yako
0 comments:
Post a Comment
Note: Only a member of this blog may post a comment.